Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Kampuni ya Shell mahakamani Uholanzi kwa kuchafua mazingira nchini Nigeria

Waakilishi wa kampuni kubwa ya mafuta ya Shell, wamefika mahakamani wakikabiliwa na mashtaka ya kuchafua mazingira nchini Nigeria.

Wakulima wanne kutoka eneo lililo na utajiri mkubwa wa mafuta la Niger Delta nchini Nigeria leo wameifikisha Kampuni hiyo kubwa ya mafuta ya Shell katika mahakama ya kimataifa ya uholanzi kujibu madai ya uchafuzi wa mzingira katika vijiji vinne nchini Nigeria.

Kesi hiyo ni moja kati kesi ambayo imekuwa ikifuatiliwa kwa karibu na vyombo mbali mbali vya habari duniani. Ikiwa wakulima hao watashinda kesi hiyo, huenda ikatoa nafasi kwa maelfu ya watu wanaodai fidia kutoka kwa makampuni kama Shell.

Wakulima hao wanasema uvujaji wa mabomba ya mafuta yanayomilikiwa na kampuni hiyo yameharibu mashamba yao na biashara ya samaki.

Wa-Nigeria hao wakiungwa mkono na wanaharakati wa mazingira kutoka Uholanzi wanataka Kampuni ya Shell ilazimishwe kusafisha mazingira na kulipa fidia kwa hasara iliyotokea huko Niger Delta.

Kesi hiyo imewasilishwa mahakamani na wakulima wanne wa Nigeria kwa ushirikiano na shirika moja la kutetea mazingira la nchini humo, Friends of the Earth.

Ni mara ya kwanza kwa kampuni kubwa ya Uholanzi inashtakiwa katika mahakama ya kiraia nchini humo kuhusiana na uharibifu uliotokea katika nchi ya kigeni.

Shell, inasisitiza kuwa haijaweza kusafisha eneo ambalo lilichafuka kutokana na shughuli zake nchini Nigeria.

Inasemekana kuwa nusu ya uvujaji wa mafuta katika eneo hilo umesababishwa na visa vya wizi.

Kesi hiyo inahusishwa na uvujaji wa mafuta uliotokea katika eneo la Ogoniland nchini Nigeria.

Wakulima wanasema kuwa mafuta yaliyovuja kutoka kwa mabomba ya mafuta ya kampuni hiyo, yameathiri mapato yao, kwa kuharibu mimea na mabwawa ya samaki.

Mmoja wa walioshtaki kampuni hiyo, Alfred Akpan, aliambia BBC kuwa mafuta yaliyovuja yaliharibu vibaya mabwawa yake 47 ya samaki na anataka fidia.

Source: BBC Swahili

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO