Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Wabunge CUF wasusia Baraza la Wawakilishi

MAWAZIRI na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kupitia Chama cha Wananchi (CUF), jana walitoka ndani ya Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi mjini hapa, wakati Mwakilishi wa Jimbo la Bububu, Hussein Ibrahim Makungu (CCM), alipokuwa akiapa.

Mawaziri na wabunge hao kupitia CUF, walitoka nje ya ukumbi huo jana asubuhi, baada ya Spika wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Ameir Kificho, kutoa taarifa ya kuapishwa kwa mwakilishi mpya na kutaja jina la Hussein Ibrahim Makungu.

Baada ya Spika Kificho kutaja jina la Makungu, wawakilishi kupitia CUF, walitoka nje ya ukumbi kwa kile kilichoelezwa kuwa, hawakubaliani na ushindi wa Makungu, kwa kuwa uchaguzi uliomweka madarakani hivi karibuni, ulikuwa na utata.

Pamoja na CUF kususia tukio hilo, Makungu aliapishwa. Soma zaidi

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO