Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

KITAMBI NOMA BIGWA BONANZA LA PASAKA ARUSHA

mkuu wa wilaya ya Hai Novatus Makunga akiwa anasalimiana na wachezaji wa timu   Mango Garden ya jijini Dar es salaam wakati walivyokuja kushiriki bonanza la kitambi noma lililofanyika katika kiwanja cha kumbukumbu ya sheikh Amri Abeid ya jijini Arusha

katika bonanza hili la kitambi noma kuliuzuriwa na watu wengi akiwemo mmbunge wa jimbo Meatu  kupitia CHADEMA Aliyevaa tisheti ya blue

Mh. Meshack Opulukwa

kulikuwepo pia na mashindano ya kukimbia na magunia  ambapo katika mashindano haya mchezaji kutoka timu ya Mango Garden alishinda

  washabiki wa timu ya kitambi noma ya jijini Arusha wakishabikia ushindi mara baada ya kushinda kukimbiza kuku

wachezaji w timu ya Benson kampani  wakivuta kamba

wadau wa timu ya kitambii noma wakiwa pamoja na mdada wa libeneke la kaskazini katika bonanza la kitambi noma siku ya pasaka

Mheshimiwa mkuu wa Wilaya ya Hai Novatus Makunga akiwa na mdada wa libeneke la kaskazini(woinde shizza Blog) wakati wa bonanza la pasaka lililoaadaliwa na timu ya kitambi noma ya jijini Arusha ambapo mkuu wa wilaya ni mwanachama wa klabu hiyo

mambo ya nyama choma nayo yalikuwepo

KITAMBI noma mabingwa wa jumla wa bonanza la pasaka lililofanyika katika uwanja wa kumbukumbu ya sheikh Amri Kaluta Abeid huku timu ya Mango Garden ya Kinondoni ikishika nafasi ya pili ikiwa ni katika kusherehekea sikukuu ya pasaka kwa michezo mbalimbali.

Bonanza hilo lililoandaliwa na Klabu ya Kitambi noma yenye maskani yake jijini hapa na kufadhiliwa na kampuni ya bia (TBL)liliwakusanya mamia ya wapenda michezo na kushudia michezo ya kukimbiza kuku,kukimbia na magunia,soka,Kunywa bia,kuvuta kamba na burudani ya muziki kwa siku nzima ya pasaka.

Akifungua bonanza hilo Mkuu wa wilaya ya Hai Novatus Makunga al;iwataka washiriki wa bonanza hilo kufahamu kuwa michezo ni afya na burudani na tunatarajia kuona burudani kutoka kwenu kwani pia nimefarijika kuwaona marafiki zangu ambao wengine walikuwa wakicheza ligi kuu lakini kwa sasa vitambi vimewanyemelea hivyo michezo ni fursa nzuri ya kuvipunguza.

Makunga akawaka washiriki na watanzania kushiriki katika michezo baada ya shughuli zao katika suala zima la kujenga Afya zao na kuleta burudani hakika taswira hiyo itajenga taifa la watu wenye Afya na kuondoa magonjwa mbalimbali yanayoinyemelea jamii yetu.

Timu zilizoshiriki katika bonanza hilo ni pamoja na Arusha Coaches,kampuni ya Benson,Mango Garden ambao walikuwa wageni waalikwa kutoka jijini Dar es salaam na wenyeji Timu ya Kitambi Noma zote za jijini Arusha ambapo katika soka timu zote zilicheza kwa mzunguko na kujikusanyia pointi na bingwa kupatikana.

Katika mechi ya kwanza kati ya Arusha coaches walifungwa bao moja bila majibu na timu ya mango garden ikifuatiwa na mechi ya wenyeji kitambi noma na timu ya bensons na kujikuta benson wakipigiliwa kwa bao mbili bila majibu mechi iliyofuata ni kati ya timu ya makocha wa mkoa wa Arusha na Benson mchezo ulioisha kwa Arusha Coaches kuwapigilia bila huruma benson kwa bao 3 bila majibu.

Kwenye mchezo wa kuvuta kamba timu ya kitambi noma iliibuka mshindi katika fainali yake na timu ya benson huku benson na kitambi noma wakiibuka washindi kwa kugawana kuku moja moja katika mashindano ya kukimbiza kuku huku bonanza hilo likifana na kuwapa burudani murua wakazi wa jiji hili na viunga wake.

PICHA ZOTE NA MAELEZO: MAMAA WA LIBENEKE LA KASKAZINI WOINDE SHIZZA

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO