Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

TASWIRA: MATUKIO MBALI MBALI YA UCHAGUZI WA VIONGOZI WA CHADEMA JIMBO LA ARUSHA MJINI

Mh Freeman Mbowe akimkabidhi Katibu (Arusha Mjini) aliye maliza muda wake ndugu Martine  Sarungi cheti cha Pongezi kwa kufanikisha Programu ya CHADEMA MSINGI

Huu ndio Uongozi  mpya wa Arusha Mjini ulio Chaguliwa katika uchaguzi huru na wa kidemokrasia. Mstari wa mbelw kutoka kushoto, Mwenyekiti Derick Magoma; Katibu wa Jimbo Bw Lewis Kopwe, Katibu Mwenezi Bw Gabriel Kivuyo,; Mweka Hazina wa Jimbo na Mjumbe wa Mkutano Mkuu Mwanasheria James Lyatuu.

Matokeo ya kura kwa nafasi mbalimbali za uongozi yalikuwa kama ifuatavyo

Wajumbe wa kamati tendaji
Daudi Safari - 60
Haika Alex - 20
Margaret Samson – 123
(amekuwa mjumbe)
Tumainiel Wilbald – 90 
(amekuwa mjumbe)
Kitumbizi Bahati – 103
(amekuwa mjumbe)
Francis Chuma – 130
(amekuwa mjumbe)
Heriery Humphrey - 20

Mjumbe wa Mkutano Mkuu Taifa
Issaya Doita - 36
James Lyatuu – 105
(amekuwa mjumbe)

Mweka Hazina
Nsajigwa Mwakatobe - 133

Katibu Mwenezi
Gabriel Lucas Kivuyo – 138


Katibu wa Jimbo
Mosses Nanyaro - 45
Lewis Kopwe-92 (Katibu)

Mwenyekiti Jimbo
Kalist Lazaro - 31
Magoma Dereck – 108 (Mwenyekiti)

 

Katibu wa Kanda Ndugu Amani Golugwa akiwaelekeza wajumbe wa mkutano mkuu taratibu na kanuni za Uchaguzi

Mh Freeman Mbowe akimkabidhi Jenipher Kauseria  cheti cha Pongezi kwa kufanikisha Programu ya CHADEMA MSINGI

Mh Freeman Mbowe akimkabidhi Francis Chuma  cheti cha Pongezi na kofia  kwa kufanikisha Programu ya CHADEMA MSINGI

Mh Freeman Mbowe akiongea na wajumbe wa mkutano mkuu wa Jimbo la Arusha Mjini,amewaeleza umuhimu wa kufanya uchaguzi sahihi wa viongozi wa ngazi ya Jimbo

Wajumbe wa mkutano mkuu wa Arusha  Mjini

Mwenyekiti Mpya wa Arusha Mjini MAGOMA DERICK MAGOMA  akishangilia ushindi alioupata katika uchaguzi wa kidemokrasia usiokuwa na rushwa, vurugu wala hujuma ya aina yeyote

Mwenyekiti Mpya wa Arusha Mjini MAGOMA DERICK MAGOMA  Akishangilia ushindi alioupata katika uchaguzi wa kidemokrasia. Picha hizi na Bw Makabayo, Ofisa wa Chadema Kanda ya Kaskazini

MATUKIO YA AWALI NA NJE YA UKUMBI

 

20140726_101617Mwenyekiti Mteue wa Jimbo la Arusha Mjini, Bw Derick Magoma katika kusalimiana na muasisi wa Chadema Mzeee Edwin Mtei wakati anawasili kufungua chaguzi za mabaraza ya chama

20140726_104058

Wagombea waliokuwa wakiwania nafasi ya kuwakilisha Jimbo kwenye Mkutano Mkuu, Mh Doita kushoto na Mwanasheria James Lyatuu wakitambiana kabala ya uchaguzi. Baadae James aiibuka mshindi kwa kura 105 kwa 36.

20140726_104215

Baadhi ya wazee wa chama wakiwasili na kusalimiana na wanachama wengine

20140726_110107

Mwanasheria James Lyatuu akifanya mazungumzo na wagombea wengine wa nafasi ya Ujumbe Kamati Tendaji; Magreth Samson na Daudi Safari

20140726_110238

Wajumbe wakitambulishana

20140726_111419

Bw George kushoto kutoka kitengo cha Intelijensia ya Chadema akibadilishana mawazo na Dereva wa Mbunge Lema, Haleluya Natai kulia na Bw Tumainiel Wilbald (katikati) ambaye amechaguliwa kuwa Mjumbe wa Kamati Tendaji

20140726_112117

20140726_112139

Baadhi ya wagombea wakikumbushia masualambalimbali ya chama kama yalivyoelekezwa na Katiba ya chama kabla ya kuingia ukumbini kujieleza mbele ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Wilaya

20140726_113119

Zoezi la Usaili wa wajumbe chini ya aliyekuwa mwenyekiti wa ijana Hai, Bi Doris Cornel. Doris kwasasa yupo likizo ya masomo akitokea nchini Switzerland

20140726_115920

Timu ya wanahabari wa Chadema Arusha wakifurahia jambo na Mwanasheria James Lyatuu kabla ya vikao vya uchaguzi kuanza

20140726_151904

Aliyechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa BAVICHA, Bw Innocent Kisanyange akihojiwa na Mwandishi Ferdnand Shayo mara baada ya kutangazwa mshindi

20140726_095425_thumb[2]

Washindani wakuu kwa nafasi ya Mwenyekiti Bw Kalist Lazaro almaarufu kama Bush (kushoto) na Derick Magoma katikamazingira ya kutambiana kabla ya uchaguzi. Hitimisho lilikuwa ni Magoma kuibuka mshindi katika nafasi hiyo ya Mwenyekiti wa Wilaya

20140726_095639_thumb[2]

Baadhi ya vifaa mbalimbali vyenye nembo ya chama vikiwa sokoni

20140726_095653_thumb[2]

Mwenyekiti mpya wa BAVICHA Wilaya Innocent Kisanyange na Katibu wake Glory Kaaya katika picha ya pamoja mara baada ya kuibuka washindi

20140726_095858_thumb[2]

Ofisa Uchaguzi kutoka ofisi ya Kanda ya Kaskazini, Bw Kingu akitoa maelekezo kwa baadhi ya wajumbe wapigakura na wagombea kala ya zoezi husika kuanza

20140726_100549_thumb[2]Mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti Wilaya ya Arusha Mjini, Bw Magoma (kulia) akisalimiana na Mbunge wa Arusha Mjini, Mh Godbless Lema

20140726_100610_thumb[2]

20140726_101035_thumb[2]

Mjumbe wa Kamati ya Chadema ni Msingi, Daniel Urioh (kushoto) kabla ya uchaguzi. Urioh aligombea nafasi ya Katibu wa Bavicha Wilaya lakini mchuano ulikuwa mkali na Glory Kaaya kuweza kuibuka mshindi20140726_101508_thumb[2]

Glory Kaaya (kulia) ambaye ameshinda nafasi ya Katibu wa BAVICHA Wilaya akifurahia jambo na aliyekuwa mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti BAVICHA Wilaya, Bw Damuni Melamari ambaye kura zake hazikutosha kumtanganza mshndi. Uchaguzi wa ngazi hiyo ulilazimu kurudiwa mara tatu ili kupata mshindi baada ya washindani kuwaribiana sana.

20140726_101635_thumb[2]

Muasisi wa Chadema, Mzee Edwin Mtei akisalimiana na wanachama mara baada ya kuwasili eneo la mkutano kuzindua chaguzi za mabaraza!

20140726_102021_thumb[2]

20140726_100656_thumb[2]

Mbunge wa Arusha Mjini akitoa maelezo yake kwa Afisa wa Kanda, Bi katika zoezi la uandikishaji wajumbe wa kushiriki mkutano husika

20140726_100442_thumb[2]

Wajumbe wawili wa Kamati Tendaji katika picha ya pamoja kabla ya uchaguzi wao kufanyika. Kushoto ni Kitumbwizi Bahati ambaye pia ni Katibu wa Redbrigade wa Chama.

 

PICHA ZOTE NA MAELEZO: SERIA WA ARUSHA255

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO