Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MBUNGE WA JIMBO LA VUNJO,JAMES MBATIA AANDAA JIMBO LAKE KUKABILIANA NA MAJANGA (NDENGA)


Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi taifa na Mbunge wa jimbo la Vunjo,James Mbatia akichokoza mada wakati wa kongamano la Elimu juu ya maafa katika jimbo hilo baada ya kukumbwa na mafuriko ,Kongamano lililofanyika katika shule maalum ya Viziwi na kuwashirikisha wenyeviti wa mitaa,Vijiji na Vitongoji,Maofisa watendaji,Madiwani,wakuu wa idara mbalimbali katika jimbo hilo.
Baaadhi ya washiriki wa kongamano hilo.
Mkuu wa Wilaya ya Moshi,Novatus Makunga akichangia mada katika kongamano hilo ambalo alikuwa mgeni rasmi pia,kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Vunjo ,James Mbatia na kulia Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Moshi,Michael Kilawila.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Moshi,Michael Kilawila akichangia mada katika kongamano hilo lililotumika pia kuondoa itikadi za kisiasa huku akitoa wito kwa viongozi wote katika jimbo hilo kufanya kazi za maenedeleo bila ya kujali itikadi za kisiasa.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Moshi,Fulgence Mponji akichangia mada katika kongamano hilo lililoandaliwa na Mbunge wa jimbo la Vunjo,James Mbatia akielea namna ambavyo Wilaya hiyo ilivyopata athari kutokana na mvua zilizonyesha Aprily 24 na 25 mwaka huu.
Mwenyekiti wa mji mdogo wa Himbo ,Hussein Jamal akichangia mada katika kongamano hilo.
Mkuu wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga,(kushoto) Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Moshi,Fulgence Mponji (katikati) na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Moshi,Michael Kilawila wakiteta jambo wakati kongamano hilo.
Baadhi wa wachangiaji katika kongamano hilo wakitoa michango yao.
Mbunge Mbatia akiteta jambo na Mkuu wa wilaya ya Moshi ,Novatus Makunga.
Washiriki wa kongamano hilo wakiwa wamejigawa kulingana na kata wanazotoka ambazo zinafikia 16 katika jimbo la Vunjo wakijadili maafa yaliyozikumba kata hizo na namna ya kukabiliana nayo kabla ya mkutano huo kutoa maazimio.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO