Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Mbunge wa viti maalum (CCM) Catherine Magige ahusishwa na tuhuma za utekaji, kulisha sumu na kujeruhi(Audio,muhusika akielezea hapa)




SIKILIZA KISA KINACHOFICHUA TUHUMA ZA MKURUGENZI WA JIJI LA ARUSHA KIHAMIA NA MBUNGE WA VITI MAALUM (CCM) CATHERINE MAGIGE WAKIHUSISHWA NA UTEKAJI, KUJERUHI NA KISHA KUMVUA VYEO MRATIBU ELIMU NGARENARO.
Audio hii hapa na maneno yake yame chapishwa hapo chini
Audio Player

Anasimulia hivi
“Kwa majina naitwa Batuli Hamad Isaya, ni Mwalimu wa Shule  ya Msingi Unga Ltd, Kata ya Unga Ltd Mkoani Arusha.
Nakumbuka ilikuwa siku ya Jumatatu tarehe 3 jioni mida ya saa  moja, nilikuwa naenda  dukani  kununua vocha simu  yangu ilikata. Kwa hiyo nikachukua hela nikaenda dukani  kununua vocha ambapo  ni barabarani. Nimefika barabarani nikanunua vocha nikaikwangua nikawa narudi nyumbani. Kutoka barabarani mpaka nyumbani  kwangu kuna uchochoro ambao ni nimrefu kidogo, nikawa nikitembea kuelekea nyumbani huku naingiza vocha kwenye simu, namulika namba naingiza, namulika namba naingiza. Nilivyofika katikati ya uchochoro kuna mkaka alikuwa nyuma  yangu, akanisalimia, anambia Batuli mambo? Nikamwambia poa. Sikuhangaika nae kwasababu niliona ni mtu  anayenifahamu.
Lakini ghafla, kwa dakika moja akanambia simama hapo ulipo na ufuate maelekezo yangu, tofauti na hapo nitakupiga shaba. Nilipata hofu nikawa nimetetemeka ghafla simu  yangu ikawa imedondoka lakini alinambia okota simu  yako. Akawa ametoa bastola amenishikia kwa mgongoni.
Baada ya hapo nikawa nimesimama kwa hofu natetemeka, akanambia usiogope, Mimi nahitaji  tu kuongea na wewe. Nitakachokuelekeza ukifuate tofauti na hapo nitakupiga shaba ya mgongo. Utarudi ulipotoka utaenda mpaka mwisho wa shule kuna Gari jekundu, utaingia kwenye hilo gari  nataka tuzungumze.
Basi, kwa ile hofu niliyokuwa nayo na kutetemeka niligeuka na kuanza  kufuata maelekezo aliyonielekeza lakini alikuwa yuko  nyuma  mimi  mbele. Nikaanza kurudi, nikarudi mpaka barabarani nikateremka chini kidogo kwenye hilo gari nikafika, akafungua mlango, akanambia niingie, kulikuwa kuna mkaka alikuwa amekaa ndani ya gari  akanipisha nikaingia nikakaa. Akafunga mlango  yeye akazunguka upande wa dereva akapanda.
Ndani ya gari  taa zilikuwa  zimezimwa lakini kulikuwa kuna wakaka wawili, mmoja alikuwa alionipisha na mwingine alikuwa amekaa upande wa kushoto. Nikawa nimekaa katikati yao.
Baada ya muda, yule kaka akawasha gari, akageuza akawa anaelekea upande wa juu.
Nikawa na hofu sana, lakini aliyekuwa amekaa upande wa kulia  kwangu akaanza kunisemesha. Akanambia, *we Batuli, ulipoenda kumshitaki Mkurugenzi wako uache mara  moja. Na hapo ulipoenda kulalamika usirudi tena, kama unapenda kazi yako kama unapenda maisha yako.* Tulia ufundishe na unyamaze ufunge mdomo kimya.
Wakati huo tulikuwa  tumefika eneo moja lina  mataa panaitwa Kona ya Esso. Nikawa nimeshtuka sana nikaendelea kupata hofu. Sasa baada ya kuniambia yale  maneno, nikawa nimepata wazo. Au kwasababu nilienda  kulalamika kwa Mkuu wa Wilaya kuhusu ishu ya Mkurugenzi? Kwa hiyo nikawa najiuliza maswali kichwani. Lakini baada ya hapo, nikaanza sasa kuhisi kwamba siko salama. Nikaanza kupiga kioo cha gari. Wakati huo tulikuwa tumefika eneo moja naiona  sheli kwa mbele, nafikiri ni maeneo ya Kona  Mbauda.
Nikawa napiga lile  gari kwa nguvu upande wa kulia,  kioo kikawa kimevunjika kwa malengo kwamba nipige kelele sasa niombe msaada.  Lakini wakati nagonga lile  gari, kioo kilivyovunjika, yule kaka aliyekaa kulia  kwangu akawa ameniwekea kiwiko cha mkono shingoni. Alivyoniwekea kiwiko cha mkono shingoni akawa amenikandamiza, nikawa najitahidi kutoa ule mkono lakini akawa tayari amenibana eneo la shingo. Kaka aliyekuwa amekaa upande wa kushoto kwangu, akawa kama vile ananisukuma kichwani, akachukua kitambaa akaniziba puani na mdomoni. Baada ya kuniziba pua na mdomo nikaanza kuhisi  kizunguzungu. Lakini baada ya muda nikawa nimeishia kwenye usingizi. Kwa hiyo sikujua tena kilichoendelea.
Lakini baadae, nikawa nahisi tena niko  kwenye gari, nasikia sauti za watu wanaongea, nikijarubu kufumbua macho nikawa nashindwa. Nikijaribu kufungua mdomo naona mdomo ni mzito. Baada tena ya muda nikaendelea kupata fahamu taratibu, baadae nikaweza kufungua macho. Ile kufungua nikakutana kuna mkaka alikuwa amekaa pembeni yangu ambaye  ni askari lakini ninamfahamu anaitwa Yuda. Alikuwa amekaa pembeni ya kitanda ni mazingira ya hospitali. Wakati huo kulikuwa kuna dokta ananicheki.
Basi wakati nimefungua macho, Yuda alikuwa anaendelea kunihoji, ilikuwaje nikawa numuelezea kwamba kulikuwa kuna watu wamenichukua wamenieleza moja mbili tatu. Wakati Yuda ananihoji dokta akawa anaendelea  kunichoma drip, akawa amenitundikia dripu na amenichoma na sindano ndio wakati huo Yuda akawa  anamueleza daktari kwamba kuna mabomba haya ya sindano tumeyakuta  hapo chini, wakawa wanayacheki baadae dokta akasema kwamba haya mabomba, hii kiboksi mlichokiokota ni kiboksi cha insulin, itakuwa  wamemchoma dawa ya sukari ya kuteremsha sukari mpaka chini. Na hapo hapo wakachukua vipimo wakanicheki sukari wakakuta kweli  sukari iko chini wakaendelea kunitundikia dripu. Nikapelekwa WODINI, baadae dokta alinicheki akanambia sijaingiliwa kwenye maumbile yangu ya kike  lakini nilikuwa nableed. Nikamuuliza hii bleed inasababishwa na nini akanambia ni hali ya hofu ndio maana bleed inatoka lakini hakuna jeraha lolote.
Ila  kwa upande wa tumboni kulikuwa na maumivu makali, kulikuwa na kijereaha ambacho kinaonekana nimechomwa na kitu chenye ncha kali, lakini manesi walivyonicheki wakasema kwamba hata  kama ni kisu au ni bisibisi, haijaingia sana ni kisehemu kidogo kama robo  sentimeta. Nikaingizwa wodini  nikaendelea kupata matibabu. Nikalala pale wodini  mpaka asubuhi.
Asubuhi daktari akapita akanicheki nilikuwa na maumivu sehemu za tumbo, akaniandikia kwamba nitafanyiwa ultra sound lakini akanianzishia kwanza antibiotic, na baadae wakanichukua vipimo vya  kunicheki maambukizi kwasababu nilichomwa na vitu vyenye ncha kali  mkononi  pamoja na maeneo ya tumbo. Wkanicheki HIV test baadae nikapelekwa kwenye chumba cha counselling nikafanyiwa counselling, wakanishauri nianze dawa  za kuzuia maambukizi kwasababu damu yangu ilikuwa iko negative. Nikakubali nikaanza hizo dawa, wakashauri nilale tena kwa siku ya pili ili waangalie kama mwili wangu utakuwa na mabadiliko  yeyote. Kwahiyo  nikabaki pale hospitali ya Mt Meru mpaka siku iliyofuatia asubuhi, nikawa niko  vizuri lakini asubuhi daktari akanishauri niendelee kutumia hizi dawa  nisifanyiwe tena ultrasound. Kama nitaonekana nina  tatizo lolote basi nitarudi kwa ajili ya vipimo zaidi. Kwa hiyo akaniandikia dawa  za kumeza antibiotic, wakanipa na hizo dawa  ambazo nilikuwa nimeshazianza jana  yake  nikaruhusiwa kwenda nyumbani.
Sasa nikawa najaribu kuwaza kwamba hili tukio kwanini litokee na kwanini wale watu waniambie hivi. Nikajaribu kuwaza sasa kuna kipindi kama wiki nne zilizopita katika idara yangu ya kazi nilipata promotion. Nilipata barua ya kuniteua kuwa Mratibu wa Elimu katika Kata ya Ngarenaro, nikaipokea, hiyo barua ilikuwa inaonesha ni tarehe 17/9/2016 nikaenda kuripoti kwenye kituo nilichoelekezwa nikaanza kazi mara  moja. Kata hiyo ina shule kama 9. Nikaanza majukumu ambayo barua ilikuwa imenielekeza. Lakini nikafanyakazi wiki la kwanza, wiki la pili, wiki la tatu.
Wiki la nne  tukiwa ndani ya kikao ambacho kiliitishwa na Mkuu wa Mkoa, Mrisho Gambo ukumbu wa AICC ambaye  aliwaita walimu wa Sekondari nikapigiwa simu  na mlinzi wangu wa Kata ambaye  ni Afisa Taaluma, Sara, akanambia unaitwa, njoo huku mbele nifuate. Nikamfuata ndani ya ukumbi, kufika pale akanambia nenda kwa Mr Mallya kuna maagizo, nikamfuata akanambia unatakiwa  urudi  kwenye kituo chako. Nikamwambia sawa. Nikajua ni maelekezo ya kazi, nikarudi kwenye kituo changu  pale nikatulia nikawa nasubiri labda kuna kitu chochote.
Mpaka saa  tisa na nusu, sikuona chochote, baadae tena nikapigiwa simu,  unaitwa Ofisi za Elimu. Nikarudi tena Ofisi za Jiji. Nilivyofika nikakutana na barua Afisa Elimu amenipa barua ya kutengua uteuzi wangu. Nikaipokea ile barua pale pale nikaifungua nikaisoma imeandikwa Kutengua Uteuzi wa Kuwa Mratibu wa Elimu Kata ya Ngarenaro. Nilipoisoma tena, kwanza nikashtuka, nikatetemeka, nikasema nimefanya nini? Ni nini nimeshindwa? Sikupata majibu sahihi, nikamuuliza Afisa Elimu hii barua ni vipi? Akasema mimi  sijui kinachotakiwa fuata maelekezo ya barua iliyokuelekeza, aliyekuteua ndio aliyekutengua.
Basi nikaipokea barua mara  moja nikarudi kituo cha kazi nikaripoti nikamuomba Mwalimu Mkuu wangu akanipangia vipindi nikaendelea na kazi. Lakini baada ya siku mbili, nilianza kujiuliza kichwani, hii nafasi ndogo nimepewa nimeshindwa kwasababu gani? Nikataka sababu zilizonisababisha  kushindwa hii kazi.
Nilichokifanya nilienda kwa Mkuu wa Wilaya ambaye  ni DC wangu, nikamuelezea kwamba, nikamshirikisha kulikoni kwamba  nimepata promotion ndani ya wiki nne  halafu wamenitengua lakini hawajanipa sababu za msingi na sielewi ni kitu gani ambacho nimekosea, napaswa kujua kwasababu Mimi nimejiendeleza, nina  skills, nina  uwezo wa kufanya kazi, sasa kama kazi kama hii ndogo nimeshindwa kufanya kazi kubwa nitawezaje na nimeshatuma application mbalimbali?
Kwakweli, Mkuu wa Wilaya akaniambia , akasoma zile barua, nikampa background kidogo ya kazi ambazo nimeshawahi kufanya, nimeshiriki kazi nyingi katika jamii, akanambia hii itakuwa ni sintofahamu, ananiambia hebu ziache hizo barua zako zote mbili nitafuatilia nijue kwa Mkurugenzi kuna sintofahamu gani. Baadae ikabidi  nimuelezee Mimi naona kama vile *Mkurugenzi wa Jiji la Arusha* Hajanitendea haki, kwasababu, kwanza alipaswa kuniambia ni kitu gani ambacho nimekosea, kitu gani ambacho nimeshindwa, yaani kipi ambacho sijakifanya mpaka aniandikie barua ya kunitengua? Lakini sikupata ushirikiano. Ushirikiano ni kwamba rudi kafanye kazi ukae kimya.
Sasa nikawa nahusianisha hii *kwenda kwa Mkuu wa Wilaya ndio imepelekea mimi  kuja  kufanyiwa  kitendo kama hiki nilichofanyiwa au ni kipi kilichosababisha?* Sikupata majibu sahihi.
Lakini baadae nikaendelea kuvuta kumbukumbu zangu ziku  za nyuma, nilivyopata hii barua ya promotion, katika haya maGrupu ya WhatsApp, ambayo niliona Mheshimiwa *Mbunge Catherine Magige alishawahi kuandika kwamba watashughulika na vyeo vyangu, watanishughulikia na wakasema kwamba hawaongei na mbwa wataongea na mwenye  mbwa* na hawakunisight kabisa jina  langu. Lakini nikafuatilia nikaona ni meseji ambazo hazina mantiki nikawa nimetulia.
Sasa baada ya kupata hili tukio la kutekwa ndio nimeanza kuhusianisha, *je, ni Mkurugenzi ndio kwasababu nimelalamika kwa Mkuu wa Wilaya ndio amesababisha hili au ni Mbunge Catherine Magige kwasababu ya kumuadvise katika kazi zake ameona namkosoa sana katika kazi zake ndogondogo?* Nimeshindwa kupata majibu.
Na mpaka kufikia sasa hivi naendelea na dawa  ambazo  zinanisababishia  kuharisha, kutapika na *Kesi hii iko Polisi kwasababu Polisi ndio  walioniokota.*
Polisi wameahidi watalishughulikia  lakini leo  nina  siku ya tisa  sijaona reaction yeyote na wameniahidi kwamba wanaendelea kufuatilia. Sasa sijajua wanafuatilia nini au sijajua ninasaidikaje kwasababu mpaka dakika hii sielewi lakini iko mikononi mwa  Polisi walishachukua maelezo, wamekuja kunitembelea, wanafuatilia. Na *hata RCO alikuja  hospitali kunisalimia* kwa hiyo bado wanafuatilia.
Kwa hiyo nilikuwa naiomba  Serikali kama itaweza  kunisaidia afya yangu niendelee kuchunguzwa kwasababu mpaka dakika hii *sina  uhakika kama sindano nilizochomwa ni kweli  ni hizo za insulin kwamba sukari ishuke au ni virusi  vya Ukimwi wameniingizia ili nife taratibu, au ni nini kimewekwa katika mwili wangu*, bado sijajiridhisha kwasababu sijachekiwa sumu  kwenye mkojo, sijachekiwa…yaani sielewi kwakweli.
Kwa hiyo ni ninaomba kwa yule ambaye  anaweza kunisaidia basi anisaidie.
Naomba pia swala hili hata Mh Rais  aweze kulifahamu kama kuna mtendaji ambaye  anaweza kuenguliwa nafasi yake  pasipo kujua kosa lolote, ni vyema akalifahamu. Ikawa ni vizuri na Mimi nikaelewa kwamba nilichofanyiwa ni haki? Uko kwenye nafasi, hujawahi kufanya kosa lolote, hujakutwa na kashfa yeyote, hujahusika na watoto hewa au hujahusika na ubadhirifu wa fedha, umetenguliwa pasipo sababu ya msingi na kila ukihoji wanakwambia kwamba nyamaza kimya endelea kufanya kazi. Nashindwa kuelewa kwakweli, bado naona Mkurugenzi wangu wa Jiji la Arusha hajanitendea haki, labda kuna sintofahamu lakini ni vyema akaiweka wazi kwasababu naona kwanza amenichafulia faili  kutokana  na nina  uwezo wa kufanya kazi. Na kazi nafanya.
Kwa hiyo kama kuna chombo cha sheria kinafuatilia kitende haki …”
CHANZO: HABARITZ.COM
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO