Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

KUTOA NI MOYO SI UTAJIRI. NAMNA YA KUCHANGIA MATIBABU TUNDU LISSU


Jinsi ya kuchangia matibabu ya mpambanaji wetu Tundu Lissu.

Ofisi ya CHADEMA Makao Makuu inapenda kuwataarifu wale wote ambao wanahitaji kutuma mchango wao wa kuchangia matibabu ya Mhe.Tundu Lissu kwamba wanaweza kufanya hivyo kupitia akaunti ya Chama yenye jina la "Chadema M4C" katika Benki ya CRDB ambayo ni: 
Benki: CRDB.
Jina la Akaunti: CHADEMA M4C.
Namba: 01J1080100600.
Tawi: MBEZI BEACH.
Huhitaji kwenda Benki,
Unaweza kuchangia kwenda kwenye akaunti hiyo ya benki kupitia huduma za M-PESA au Tigo Pesa na au Airtel Money kama ifuatavyo:

1. Kuchangia kupitia M-PESA
Piga: 150*00# chagua 6 - Huduma za Kifedha, kisha chagua 2 - M-PESA kwenda Benki kisha chagua 1 CRDB na kisha 1 weka namba ya akaunti ambayo ni 01J1080100600.
Baadaye malizia kwa kufuata maelekezo

2. Kuchangia kupitia Tigo Pesa

Piga: *150*01# chagua 6 - Huduma za Kifedha, kisha chagua 1 Tigo pesa kwenda Benki, kisha chagua 1 CRDB na kisha 1 kuingiza namba ya kumbukumbu ambayo ni 01J1080100600.
Baadaye malizia kwa kufuata maelekezo.

3. Kuchangia kupitia Airtel Money
Piga *150*60# chagua 1 Tuma Pesa, kisha chagua 1 Tuma kwenda Benki kisha chagua 2 CRDB Bank na kisha 1 ingiza namba ya akaunti ambayo ni 01J1080100600.
Baadaye malizia kwa kufuata maelekezo.

Aidha, unaweza kutuma moja kwa moja mchango wako kwa njia ya M-PESA kupitia namba 0759865786 yenye jina la "Ester Matiko" Mbunge wa jimbo la Tarime mjini kupitia CHADEMA.
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO