Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

HATIMAYE WAKILI NYAGA MAWALLA AZIKWA LEO

DEATH AND FUNERAL ANNOUNCEMENT

Familia ya Wakili Nyaga Mawalla imeridhia ndugu yao azikwe jijini Nairobi, Kenya na kumaliza mvutano wa suala la mazishi ya wakili huyo.Mawalla alifariki dunia jijini Nairobi baada ya kuanguka kutoka kwenye ghorofa katika hospitali alikokuwa akitibiwa Machi 23, mwaka huu.


Hata hivyo, kulizuka mvutano wa mazishi yake baada ya Wakili Fatuma Karume kupeleka wasia wa marehamu uliokuwa umeelekeza kuwa ikitokea amefia nje ya nchi azikwe huko au akifia ndani ya nchini basi azikwe kwenye shamba la Momella, Arusha wakati wazazi wake walitaka azikwe kwao Marangu mkoani Kilimanjaro.


Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Dar es Salaam jana msemaji wa familia hiyo, Joseph Nuwamanya alisema wameamua kuheshimu wasia wa marehemu.


“Familia na ndugu wote wa mpendwa wetu Mawalla wameamua marehemu azikwe Jumatano jijini Nairobi kwani kabla ya kifo chake yeye mwenyewe alitaka azikwe sehemu atakayofia ikitokea amefia nje ya nchi,”alisema Nuwamanya. Alisema licha ya ndugu yao kuzikwa huko taarifa zaidi kuhusiana na sehemu, muda wa mazishi zitatolewa pindi utaratibu utakapokamilika.


Akizungumzia sababu za kifo chake alisema taarifa rasmi ya sababu za kifo chake bado hazijatolewa na uongozi wa Hospitali ya Nairobi kutokana na kutokamilika kwa uchunguzi unaoendelea.
“Kumekuwa na taarifa zinazopotosha kuhusiana na kifo chake lakini nataka niseme kwamba taarifa rasmi bado haijatolewa kwani uchunguzi unaendelea na zitakapokuwa tayari kila kitu kitaelezwa,”alisema.


Nuwamanya aliwashukuru watu wote walioshirikiana nao katika kipindi chote cha msiba na kwamba alivitaka vyombo vya habari kushirikiana na familia pamoja na ndugu katika kipindi hiki kigumu.Alisema baada ya mazishi, Alhamisi itafanyika misa ya shukrani sehemu ambayo itatangazwa badaye.


Kifo cha Mawalla kilitikisa kutokana na ukweli kuwa wakili huyo alijitengenezea jina kubwa kutokana na shughuli zake mbalimbali.


Mawalla pia alikuwa anasimamia kampuni mbalimbali zilizokuwa zinawekeza nchini na hasa katika sekta ya upangishaji nyumba na ofisi. Wakili huyo pia alikuwa mdau katika sekta ya uwindaji, ambayo usimamizi wake mara nyingi umekuwa na utata mwingi na hasa katika ugawaji wa vitalu.


Alikuwa pia mshiriki wa sekta ya utalii na alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wanaunga mkono ujenzi wa Uwanja wa Mugumu huko Serengeti.

Balozi Kagasheki kuongoza mazishi ya Wakili Mawalla

Moshi. Vigogo mbalimbali wakiwamo mawaziri na wabunge wanatarajiwa kushiriki mazishi ya Wakili mashuhuri nchini, Nyaga Mawalla yatakayofanyika leo jijini Nairobi, Kenya.

Miongoni mwa vigogo hao ni Waziri wa Utalii na Maliasili, Balozi Khamis Kagasheki, Naibu wake, Lazaro Nyalandu na Mwenyekiti wa Chadema ambaye pia ni Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe.

Taarifa ya Wakili Albert Msando ambaye ni miongoni mwa mawakili wa marehemu iliyotumwa kwa gazeti hili kutoka Nairobi, ilisema katika orodha hiyo wamo wabunge na wakuu wa kampuni mbalimbali.

Wabunge watakaohudhuria mazishi hayo ni mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nasari, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema na Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa.

Watu wengine mashuhuri watakaohudhuria mazishi hayo ni Jaji Mark Bomani, Sir George Kahama, Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Dk Batilda-Salha Buriani na familia ya marehemu wakiwamo wazazi.

Licha ya viongozi na watu mashuhuri kuthibitisha kuhudhuria mazishi hayo, wapo ndugu, jamaa na marafiki na waandishi wa habari watakaoondoka kwa magari maalumu ya kukodi leo alfajiri.

Wakati vigogo hao wakithibitisha kushiriki mazishi hayo, uchunguzi uliofanywa na madaktari (postmoterm) jijini Nairobi, umebainisha mwili ulikuwa na majeraha makubwa ya ndani.
Kwa mujibu wa Wakili Msando aliyepo Nairobi, uchunguzi huo uliofanyika Jumatatu iliyopita na kubaini Wakili Nyaga alipasuka ini na mapafu na kuvunjika mbavu kutokana na kuanguka.
Marehemu anayetajwa kuwa na utajiri wa kutisha hadi kuitwa ‘Bilionea Kijana’, alifariki dunia Ijumaa Februari 22, mwaka huu hospitali alikolazwa jijini Nairobi kwa kile kinachodaiwa kujirusha kutoka ghorofani.

Hata hivyo taarifa nyingine zinadai huenda aliuawa kwa kusukumwa kutoka ghorofa ya kwanza, ambako wodi yake ilikuwapo na kutokana na utata huo, polisi nchini Kenya wameanzisha uchunguzi.

Kuhusu ratiba ya mazishi, Wakili Msando alisema mazishi yake yatafanyika leo saa 8:00 mchana katika makaburi ya Lang’ata, Nairobi Kenya. Mawalla aliacha wosia ambao umefuatwa na familia.

Chanzo: Mwananchi

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO