Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Taswira: Ziara ya Waziri Mwakyembe Mkoani Arusha

Waziri wa habari, utamaduni,sanaa na michezo Dokta Harrison Mwakyembe amewataka wajasiliamali wa vinyago kutafuta zaidi soko la bidhaa zao za asili ili kukuza kipato na kuendelea kutangaza utalii wa utamaduni.

Ameyasema hayo alipokuwa akuzunguza na wajasilimali wautalii wa utamaduni katika soko la Masai,jiji Arusha.Amesema bidhaa za utalii wa utamaduni ni nembo tosha yakutangaza nchi yetu.

“Ni kweli kuna Changamoto katika ujasiliamali huu wa utalii wa utamaduni hususani kwenye tozo mbalimbali mnazotozwa na mamlaka husua.”

Serikali ipo tayari kwenye mchakato wakutatua Changamoto hii ya tozo na kuona ni namna gani soko la vinyago nchini Tanzania linakuwa na kujulikana zaidi kimataifa, kuliko kwa sasa soko kuu linajulikana lipo jijini Nairobi wakati wazalishaji wakubwa ni  watanzania.

Dokta Mwakyembe alikuwa kwenye ziara ya siku 3 Mkoani Arusha,ambapo ameweza kufungua redio mpya ya kijamii (TBC FM),aliweza kutembelea kituo cha redio cha Sunrise,alifungua mkutano wa maafisa habari na mawasilino serikali,ameweza kukutana na wadau wa utamaduni,sanaa na michezo na ameweza kutembelea soko la vinyago la jijini Arusha.

Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dokta Harrison Mwakyembe,akimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel Daqarro akimwelezea namna soko la vinyago linavyofanya kazi, pembeni ni Mwenyekiti wa soko hilo Elias Rajabu.


Waziri Mwakyembe akizungumza na baadhi ya watalii waliofika katika soko la vinyago,jijini Arusha.


Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Dokta Harrison Mwakyembe akitazama moja ya bidhaa zinazopatikana katika soko la vinyago jijini Arusha


Waziri wa Habari ,Utamaduni, Sanaa na Michezo Dokta Harrison Mwakyembe, akipokea zawadi ya kikombe kilichotengenezwa kwa shanga kwa mmoja wa wajasiliamali wa soko la vinyago jijini Arusha.


Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO