Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

LEMA:MAKONDA ANAJUA ALIPO SAA NANE


tmp_706-FB_IMG_14917446528991000571384.jpg

Mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbles Lema amesema kuwa mkuu wa mkoa wa Dar es salam Makonda anajua aliko Ben saanane hivyo awajibike kumleta.

Akizungumza na waandishi wa habari  Jana jijini Arusha Lema alisema jeshi la  polisi ndio lenye dhamana ya kufanya uchunguzi wa kina katika matukio ya watu kupotea na siyo mkuu wa mkoa.

Aidha Lema alisema kitendo cha mkuu wa mkoa wa Dar es salaam kutoa tamko la  kuhakikisha kupatikana kwa Msanii Roma Mkatoliki  kabla ya jumapili kimedhihirisha wazi kuwa anahusika na kutekwa  kwa Msaidizi wa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo  Beni Saanane.
"Watawala wanajua alipo Beni Saanane kama ambavyo makonda alijua alipo  Roma Mkatoliki  tunataka  watuletee akiwa hai ama akiwa amekufa watuletee mifupa yake" alisema Lema.
Alisema Mkuu  wa mkoa wa Dar es salaam amekuwa  msemaji wa nchi  wakati maswala ya mtu kutekwa au kupotea  alitakiwa kuzungumzia  Waziri wa mambo ya ndani Mwigulu Nchemba jambo ambalo amekaa kimya.

"Siro  alisikika  akisema  kuwa Roma Mkatoliki hayupo mikononi wa Polisi , wakati huo huo Mkuu wa mkoa akatoa tamko kuwa kabla ya Jumapili Roma atakuwa amepatikana ninani amempa mamlaka  Mkuu huyo  kuwa msemaji wa Polisi" alihoji Lema.

Alisema ni dhahiri kuwa Waziri wa Mambo ya ndani ama ameshindwa kazi au anajua mambo yanakoendelea ila anahofia kukutwa na  kilichomkuta aliyekuwa waziri wa habari,Utamaduni, Sanaa na michezo  Nape Nnauye  hivyo anaamua kunyamaza.

"Tuendako sasa  mheshimiwa Rais ammpe Uwaziri wa mambo ya ndani Makonda maana amekuwa akiingilia jeshi la  polisi katika utendaji wake jambo ambalo halimhusu" alisema.

Alisema ipo  siku ambayo hawatakuwa chadema , CUF, au CCM wananchi hawa wanaoonewa watakataa  kutekwa  ambapo alisema inaweza  kuleta machafuko nchini

Aliongeza kuwa yeye Mwenyewe anatembea kwa hofu ambapo alisema nchi haiko salama kutokana na matukio ya utekwaji yalivyoshamiri  hii ikiwa inasababishwa na watu kutotakiwa kusema ukweli.

"Nimejipanga kuhamasisha maaandamano nchi nzima katika vyuo ya kutaka vijana waandamane kutafuta alipo  Saanane, kuna wangapi wamepotea hatujui walipo  tukiendelea kukaa kimya watatekwa  wengi zaidi" alisema.

Aliongeza kuwa ni takribani miezi 6 tangu kukamatwa kwa Beni  na hadi sasa Chama chao pamoja na wazazi wake  hawajui alipo  ambapo alisema taarifa walizozipata   ni kuwa Makonda anajua alipo  Saanane.

"Tunamtaka Makonda aseme Ben alipo  la  sivyo nchi inakwenda pabaya Mimi, Mbunge wa Kigoma mjini Zito Kabwe na Mheshimiwa Tundu Lisu wa Singida Mashariki tumekubaliana kulivalia njuga suala hili kwa gharama yoyote tunamtaka hai au kama kafa tupewe mifupa yake" Alisema

Alisema kazi ya Usalama wa Taifa ni kuhakikisha Usalama wa nchi upo vizuri  na ni lazima  watakuwa wanajua haya mambo ya watu kutekwa kwani kazi yao kubwa nikulinda Usalama wa Taifa kwa ujumla.

Lema awashukia TRA Arusha.
Katika hatua nyingine Mbunge huyo ameitaka Mamlaka ya ukusanyaji  wa mapato TRA  kuacha kuwanyanyasa wafanyabiashara katika kuwadai kodi kwa kutumia silaha.

Alisema kuna watu wanatumia dhana ya Mkuu wa nchi ya ukali wake  kujipatia rushwa kutoka kwa wafanya biashara jambo ambalo amesema rushwa katika ofisi nyingi sasa inaendeshwa kimfumo .

Alisema  wafanya biashara kwa sasa wamekuwa waoga kutokana  na vitisho wanavyopata kutoka kwa watu wa TRA wanaoenda  kukagua hadi mauzo kwenye droo  za wafanyabiashara hao kwa kutumia maafisa Usalama na takukuru.
" Rais wetu ukali wako na usiriazi wako watu wachini wanautumia vibaya na wanajipatia rushwa kwa kutumia ukali ulionao   kwa kuwaogopesha wananchi  ili wawape rushwa" alisema.

Hata hivyo Lema alisema Mkoa wa Arusha unaongoza kwa  TRA kuwaonea wafanya biashara ambapo alisema yeye kama Mbunge aliyechaguliwa na wananchi atahakikisha anasimamia jambo hilo ili wafanya biashara wasiendelee kunyanyaswa.

Utaratibu wa ukusanyaji  mapato hauitaji kutumia njia za bunduki kutishiwa hadi kwenye bar, hapana hili ni jambo la  kiungwana unapomfuata mtu kiungwana anakuelewa siyo kutishia kwa kuongozana na Usalama wa Taifa ,askari polisi takukuru na  TRA " alisema.

Alisema maduka mengi yamefungwa kutokana na utaratibu mbaya wa kukusanya mapato ambao umekuwa ukiwaogopesha wafanya biashara wengi.
CREDIT: WOINDE SHIZZA
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO