Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

TANZANITE ONE KUJENGA UPYA SHULE YENYE MADARASA MANNE NA WANAFUNZI 1126


Mkurugenzi mwenza wa Tanzanite One,Faisal Juma pamoja na viongozi wa serikali na wajumbe  wa kamati ya shule ya Songambele  akikagua madarasa ambayo hayatumiki  kutokana na nyufa baada ya shule kukumbwa na mafuriko na kutangaza kujenga madarasa  saba.




Mkurugenzi mwenza wa Tanzanite One,Faisal Juma akizungumza katika mkutano na wazazi wa shule ya msingi Songambele  ambayo ina uhaba wa madarasa na kutangaza kujenga madarasa  saba Mwaka huu ili kupunguza tabu waipatayo wanafunzi hao kwa kukoisa vyumba vya madarasa.

ANDREA NGOBOLE; PMT
Siku tatu baada ya kuripotiwa shule ya msingi Songambele iliyopo Mererani wilaya ya Simanjiro, yenye wanafunzi 1126 kusoma katika madarasa manne,Kampuni ya Tanzanite One imetangaza kujenga madarasa saba ili kuondoa uhaba wa madarasa katika shule hiyo.

Mkurugenzi mwenza wa kampuni ya Tanzanite One,Faisal Shabhai amesema,baada ya kuona kwenye vyombo vya habari shida ya madarasa katika shule hiyo,wameamua kujitokeza kujenga shule hiyo.

Shabhai alisema,Tanzanite one kama mwekezaji Katika migodi ya Tanzanite wanawajibu wa kusaidia masuala ya kijamii hasa kwa kuwa wananufaika na madini ya Tanzanite.

"Tunajua tunawajibu wa kusaidia jamii hivyo tutajenga madarasa  saba katika shule hii"alisema

Katibu Tawala wa wilaya ya Simanjiro,Zuwena Omar  alishukuru kampuni Tanzanite One kwa msaada waliotoa kujenga madarasa hayo.

Omar alitoa wito kwa wawekezaji wengine waliopo Mererani kusaidia maendeleo ya Mererani.

Mwalimu Mkuu shule hiyo.Mwanahamisi Mussa alisema wanakabiliwa na tatizo la uhaba wa madarasa, matundu 40 ya vyoo,Nyumba za walimu na ofisi kwani wanafanyakazi chini ya miti.

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO