Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

TASWIRA: MKUTANO MKUU WA CHADEMA WILAYA YA ARUSHA MJINI

SAM_2690

Mkutano huu ulifanyika jana tarehe 10/05/2014 katika ukumbi wa NEW SAFARI HOTEL Jijini hapa na kuhudhuriwa na Katibu wa Kanda ya Kaskazini ammbaye pia ni Katibu wa Mkoa wa Arusha, Mh Amani Golugwa, Mbunge wa Arusha Mjini Mh Godbless J Lema, Naibu Meya wa Jiji la Arusha, Prosper Mh Msofe na Madiwani wote wa Chadema Arusha Mjini pamoja na Viongozi wa Kata zote 19 za Arusha Mjini.

Wajumbe waliohudhuria Mkutamo mkuu wa Wilaya ya Arusha Mjini

Mh Diwani Viola wa Kata ya Lemara (Viti Maalumu) akielezea mafanikio waliyoyapata katika Halmashauri ya Arusha Mjini baada ya kuweza kusimamia kikamilifu

Katibu waKanda ya Kaskazini Ndugu Amani Golugwa akiongea na wajumbe wa mkutano mkuu wa wilaya,amewahamasisha umoja na mshikamano katika ujenzi wa Chama ndani ya Arusha Mjini na nje ya Arusha,

 


Mbunge wa Arusha Mjini Mh Godbless Lema akiwakumbusha wajumbe wajibu wao katika kuwatumikia wananchi pia akielezea nikwajinsi gani watu wa Arusha walivyochangia ujenzi wa chama katika nchi yetu kwa kuwajengea ujasiri wa kutetea haki zao

PICHA: CHADEMA KANDA YA KASKAZINI


Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO