Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

TASWIRA: MUONE REDDS MISS TANZANIA 2013 NA JINSI ALIVYOPATIKA MALIMANI CITY USIKU WA KUAMKIA LEO

FKB_1224

HATIMAYE kitendawili cha nani atanyakua taji la Redd’s Miss Tanzania 2013 kimeteguliwa usiku huu na mrembo Happiness Watimanywa kutoka Mkoa wa Dodoma na Kanda ya Kati kufanikiwa kutawazwa Mshindi wa taji hilo na kuwashinda warembo wengine 29 waiokuwa wakiwania taji hilo.

Nyota ya Happiness ilionekana dhahiri kung’aa vyema katika fainali hizo mwaka huu tangu pale alipofanikiwa kutwaa taji la Miss Tanzania Photogenic 2013 na kuwa mrembo wa kwanza kuingia nusu fainali.

Wakati Happiness akinyakua Taji hilo pamoja na zawadi ya Gari na kitita cha shilingi Milioni 8 nafasi ya pili ilikwenda kwa mrembo Latifa Mohamed kutoka Kitongoji cha Kigamboni na Kanda ya Temeke na nafasi ya Tatu ikienda kwa Miss Tanzania Sports Woman, Clara Bayo.

Pamoja nao warembo wengine walio ingia hatua hiyo ya tano bora ni Lucy Tomeka na Elizabeth Prety.

Fainali za Miss Tanzania 2013 ndio zinaendelea usiku huu ndani ya Mlimani City jijini Dar es Salaam. Gari ndo hilo hapo Je nani ataingia ndani na kuliendesha? Tusubiri Majaji. Hadi sasa Top 5 ndo ishatajwa.

PICHA NA STORI: FATHER KIDEVU

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO