Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MAWAZIRI WAPYA WATAJWA: YUPO MIGIRO, JUMA NKAMIA ,MWIGULU NCHEMBA NA JENISTA MHAGAMA


Wakati ikiwa imesalia miezi 22 kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa Serikali mwaka 2015, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, amewahamisha na kuwateua baadhi ya Mawaziri na Naibu Mawaziri kama kuziba nafasi zilizo achwa wazi huku wengine wakibadilishwa maeneo yao ya kazi.

Akitangaza mabadiliko hayo leo, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue amesema Rais Kikwete amewatupa nje viongozi kadhaa akiweomo Waziri wa Mazingira, Dk. Theresia Huvisa pamoja na Manaibu waziri, Goodluck Ole Medeye aliyekuwa Ardhi, Philipo Mulugo- Elimu, Benedict Ole Nangoro- Naibu Mifugo na Uvuvi. 

Akiulizwa swali na wanahabari juu ya kuendelea kuwapo kwa mawaziri 'Mizigo' ambao walilalamikiwa na Bunge na hata vyama vya siasa, Balozi Sefue alidai kuwa hilo linatokana na namna gani Wizara iliwezeshwa katika kutekeleza majukumu yake.

Mabadiliko na uteuzi huo kamili ni kama ifuatavyo:-

OFISI YA RAIS

Hakuna mabadiliko.

OFISI YA MAKAMU WA RAIS

Waziri wa Nchi (Muungano) – Hakuna mabadiliko

Mhe. Eng. Dr. Binilith Satano MAHENGE (Mb)

Waziri wa Nchi (Mazingira).

Mhe. Ummy Ali MWALIMU (Mb)

Naibu Waziri

OFISI YA WAZIRI MKUU

Hakuna mabadiliko

WIZARA:

WIZARA YA FEDHA

Mhe. Saada Mkuya SALUM (Mb) – Waziri wa Fedha

Mhe. Mwigulu Lameck NCHEMBA (Mb) – Naibu Waziri wa Fedha

Mhe. Adam Kighoma Ali MALIMA (Mb)- Naibu Waziri wa Fedha

WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA

Hakuna mabadiliko

WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

Mhe. Dkt. Asha-Rose Mtengeti MIGIRO (Mb)-Waziri wa Katiba na Sheria

Naibu Waziri – Hakuna mabadiliko

WIZARA YA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI

Hakuna mabadiliko

WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA

Waziri – Hakuna mabadiliko

Mhe. Janet Zebedayo MBENE (Mb) – Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara

WIZARA YA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA

Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi (Mb)- Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

WIZARA YA UJENZI

Hakuna mabadiliko

WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Mhe. Mathias Meinrad CHIKAWE (Mb)- Waziri wa Mambo ya Ndani

Naibu Waziri – Hakuna Mabadiliko

WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII

Mhe. Dkt. Seif Seleman RASHIDI (Mb)- Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii

Mhe. Dkt. Kebwe Stephen KEBWE (Mb)- Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Waziri: Hakuna mabadiliko

Mhe. Jenista Joakim MHAGAMA (Mb) – Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi

WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

Waziri: Hakuna mabadiliko

Mhe. Dkt. Pindi Hazara CHANA (Mb) – Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto

WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI

Mhe. Dkt. Titus Mlengeya Dismas KAMANI (Mb) – Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi

Mhe. Kaika Saning’o TELELE (Mb)- Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi

WIZARA YA KAZI NA AJIRA

Hakuna mabadiliko

WIZARA YA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA

Hakuna mabadiliko

WIZARA YA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI

Waziri – Hakuna mabadiliko

Mhe. George Boniface Taguluvala SIMBACHAWENE (Mb) – Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

WIZARA YA MAJI

Waziri – Hakuna mabadiliko

Mhe. Amos Gabriel MAKALLA (Mb)- Naibu Waziri wa Maji

WIZARA YA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA

Waziri – Hakuna mabadiliko

Mhe. Godfrey Weston ZAMBI (Mb) – Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika

WIZARA YA UCHUKUZI

Hakuna mabadiliko

WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO

Waziri – Hakuna mabadiliko

Mhe. Juma Selemani NKAMIA (Mb) – Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

Mhe. Lazaro Samuel NYALANDU (Mb)-Waziri wa Maliasili na Utalii

Mhe. Mahmoud Hassan MGIMWA (Mb)-Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii

WIZARA YA NISHATI NA MADINI

Waziri – Hakuna mabadiliko

Naibu Waziri (Madini) – Hakuna mabadiliko

Mhe. Charles Muhangwa KITWANGA (Mb)

Naibu Waziri (Nishati)

Balozi Ombeni Y. Sefue (Pichani juu).

KATIBU MKUU KIONGOZI

Ikulu

DAR ES SALAAM

19 Januari, 2014

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO