Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Taswira: Ally Bananga Ang’ara Mkutano wa Kamepeni Chadema Kata ya Sombetini hii leo huku Lema akizidi Kukemea chuki za Udini na Ukabila

Lema na Bananga

Mbunge wa Arusha Mjini ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu Chadema, Mh Godbless Lema akimpa wosia mgombea wa chama hicho katika kinyang’anyiro cha kuwania udiwani Kata ya Sombetini katika mkutano mkubwa uliofanyika hii leo katika viwanja vya Mbauda Sokoni.

umatiSehemu ya umati wa wananchi waliohudhuria mkutano huo

Sombetini

Lema jukwwaniLema akiwa jukwaani

BanangaMh Godbless lema akimnadi mgombea wa Chadema kata ya Sombetini, Kamanda Ally Bananga

KishoaKamanda wa Chadema kutoka Iramba, mwanadada Jesca Kishoa akitambulishwa jukwaani na Mh Lema katika mkutano huo

Kishoa

Alipopata fursa ya kuzungumza, Bi Jesca Kishoa aliielezea na kuisifu Arusha na watu wake ni chachu ya mabadiliko nchini na kwamba hata historia ya nchi inaeleza hivyo. Akasisitiza zaidi na kusema kwamba kama kuna mtu anapingana na upepo huu wa mabadiliko atakuwa ni sawa na abiria wa ndege kaachwa na ndege sasa anakodisha baiskeli ili akimbize ndege, jambo ambalo halitamuwezesha kuiwahi ndege, sawasawa  na ambavyo alidai mabadiliko hayazuiliki.

DSC_0063“Amsha amsha” ya nyumba kwa nyumba, gari kwa gari, mtaa kwa mtaa ikiongozwa na Mh Lema sambamba na mgombea Bananga wakikatiza mitaa ya Mbauda

DSC_0067Maandamano kuelekea ilipo ngome ya Chadema eneo la Ngusero, Sombetini

DSC_0077Mbunge wa Arusha Mjini na viongozi wengine wakiserebuka nyimbo za hamasa zilizokuwa zinapigwa katika ngome yao Sombetini jioni ya leo

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO