Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Tamasha la Tukuza Utalii Tanzania lazinduliwa Jijini Arusha


div class="separator" style="clear: both; text-align: left;"> Na.Vero Ignatus Arusha.

Katibu mkuu baraza la Sanaa Tanzania  amewataka wazazi na walezi wa hapa nchini  kuwalea watoto na kuhakikisha kuwa wanaishi katika maadili ili kuzuia mmomonyoko wa maadili.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa tamasha la kwanza la Tanzania Tukuza Utalii Genesis 1,Godfrey Ngereza alisema kuwa tanzania imebarikiwa kwa tunu mbali mbali hivyo watanzania hawana budi kuzitunza na kuzilinda.

Aidha alisema kuwa wazazi hawana budi kuwafundisha watoto uzalendo na kuhakikisha kuwa tamaduni zilizopo haziishi.

"Waswahili walisema samaki mkunje Angali mbichi tukiwalea watoto vizuri ni ngumu kuona maadili yanamomonyoka kwa kuwa tutakuwa tumetengeneza watoto wema" Alisema Godfrey

Kwa upande wake Raisi wa Mtandao wa wasanii wa nyimbo za Injili Tanzania(TAGOANE)Dkt.Godwin Maimu Nnyaka alisema kuwa watoto yatima hawahitaji mavazi na chakula peke yake bali kujengewa msingi bora wa maisha yake.

Dkt.Nnyaka alisema wakati umefika wazazi kuwalea watoto katika misingi ya Imara na kuhakikisha wanakuwa wazalendo.

Aidha alisema kuwa kupitia tamasha hilo litasiadia kujenga vijana wenye hofu ya Mungu na kurejesha uzalendo na maadili kwa vijana.

Nao baadhi ya Washiriki akiwepo mmiliki wa kituo cha faraja Ophanage Faraja Maliaki aliishukuru TAGOANE na kuwataka wadau wengine kuungana na watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu kuwapa faraja kwa kuwa nao wanastahili kuheshimiwa kama watoto wengine.

Katibu mkuu mtendaji Baraza la sanaa nchini( Basata)Godfrey Mngereza akiwa anazungumza katika ufunguzi wa Tamasha hilo.Picha zote kwa Idhini ya Vero Ignatus Blog
Rais wa Mtandao wa Wasanii wa wasanii wa Muziki wa Injili Tanzania na maandili nchini Tanzania (TAGOANE) Dkt.Godwin Maimu akiwa anazungumza katika ufunguzi wa Tamasha la Tukuza utalii Tanzania lililozinduliwa rasmi Jijini ArushaPicha kwa idhini ya Vero Ignatus Blog
Baadhi ya watoto waliokuwa wanaishi katika mazinhira hatarishai na baadae wakachukuliwa na kupelekwa kwenye vituo vya kulelea watoto yatima.Picha kwa idhini ya Vero Ignatus Blog
Rais wa Tagoane Dkt.Godwin Maimu akiwa anacheza pamoja na watoto katika Tamasha lililoandaliwa la Tukuza Utalii Tanzania lililoandaliwa na Tagoane.Picha kwa idhini ya Vero Ignatus Blog
Mgeni rasmi Katibu Mkuu mtendaji kutoka Baraza la sanaa nchini (BASATA) pamoja na Rais wa Tagoane nchini wakikata keki kama ishara ya Ufunguzi wa Tamasha la Kuza Utalii Tanzania .
Picha kwa idhini ya Vero Ignatus Blog
Shamrashamra zikiendelea 
 Watoto wanaolelewa katika Kituo cha Faraja wakiwa katika picha ya pamoja  wakiwa na mlezi Faraja Maliaki,wapo zaidi ya watoto 200 katika ukubi wa Club D Jijini Arusha.

Mgeni rasmi kutoka Baraza la sanaa la Taifa (Basata)Godrey Mngereza akifurahi pamoja na watoto yatima katika tamasha lililoandaliwa na Tagoane Jiiini Arusha.
Wakila chakula pamoja na watoto katika Tamasha 
Meza kuu Rais wa Tagoane,Katibu Mkuu mtendaji kutoka Baraza la Sanaa nchini (Basata)Katibu mkuu Tagoane,na wakurugenzi wa vituo vya kulelea watoto yatima Jijini Arusha.Picha kwa idhini ya Vero Ignatus Blog
Muimbaji wa nyimbo za Injili kutoka Jijini Dar es salaam Gifted Wilson akiimba katika uzinduzi wa tamasha la Tukuza Utalii Tanzania Genesis 1 Jijini  Arusha.Picha kwa idhini ya Vero Ignatus Blog
Muimbaji wa nyimbo za Injili Miriam Makunja kutoka Arusha akiimba. Picha kwa idhini ya Vero Ignatus Blog
Muimbaji Wolter Chilambo kutoka Jijini Dar es salaam akiwa anaimba katika Tamasha hilo.Picha kwa idhini ya Vero Ignatus Blog

Hellen Masai akutoka Arusha kiimba .Picha kwa idhini ya Vero Ignatus Blog
Katibu mtendaji  wa Baraza la sanaa la Taifa akiwa anafurahia kwenye ufunguzi wa Tamasha la Tukuza Utalii Tanzania likilofanyika Jijini Arusha.Picha kwa idhini ya Vero Ignatus Blog
Katibu mkuu mtendaji wa Baraza la sanaa Nchini (Basata)wa kwanza kushoto akiwa pamoja na Rais wa Tagoane katika uzinduzi wa Tamasha la Tukuza Utalii Tanzania.Picha kwa idhini ya Vero Ignatus Blog
Watoto wakionyesha mavazi ya ubunifu chini ya Mwanamitindo mbunifu Diana Magesa kutoka Mwanza,Picha kwa idhini ya Vero Ignatus Blog

Picha za watoto yatima waliohudhuria katika tamasha la Tukuza Utalii Genesis 1 lililofanyika Jijini Arusha.Picha kwa idhini ya Vero Ignatus Blog

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO