Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Utata umezidi kugubika kura mbili zilizowezesha kupitishwa kwa Katiba Inayopendekezwa; Theluthi 2 Zanzibar ni ya Kufoji

Dar es Salaam.

Utata umezidi kugubika kura mbili zilizowezesha kupitishwa kwa Katiba Inayopendekezwa ambayo wiki iliyopita ilikabidhiwa kwa Rais Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein mjini Dodoma.

Utata huo unatokana na kura za wajumbe wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) upande wa visiwani, wajumbe waliokuwa Hijja, Saudi Arabia na zile za baadhi ya wajumbe wanaodaiwa kuhamishwa kinyemela kutoka Bara kwenda Zanzibar au kinyume chake.

Utata Saudia

Chanzo chetu kutoka Dodoma kilisema: “Kuna utata maana hakuna uhakika iwapo kweli mahujaji ambao ni wajumbe wa Bunge la Katiba walipiga kura maana kuna barua ilitoka ubalozini Saudi Arabia ikisema hilo lisingewezekana.”

Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa Ubalozi wa Tanzania Riyadh, uliandika barua kwa Bunge Maalumu la Katiba ukieleza kwamba usingeweza kuratibu upigaji kura kutokana na mazingira halisi ya ibada ya Hijja.

Miongoni mwa sababu zilizotolewa na ofisi ya ubalozi huo ni kwamba mtu yeyote ambaye si hujaji hakuwa anaruhusiwa kuingia katika maeneo ya Hijja na Serikali ya Saudi Arabia ilikuwa imetoa vitambulisho maalumu kwa mahujaji tu.

Katibu wa Bunge Maalumu, Yahya Khamis Hamad alikiri kupokea barua kutoka Ubalozi wa Tanzania uliopo Riyadh, ukieleza kwamba mazingira yasingeruhusu wajumbe hao wanane kupiga kura, lakini akasema walitumia njia nyingine kufanikisha kazi hiyo.

“Tulipokea barua hiyo kweli na pengine niseme tu siyo moja, zilikuwa barua kama tatu au nne hivi, maana hata hapa foreign (Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa) Dar es Salaam walituandikia kuhusu ugumu wanaouona, lakini baada ya kuona hivyo tuliamua kutumia njia zetu wenyewe.

“Tulimtuma ofisa wetu kwenda Saudi Arabia na tulimkatia tiketi na kusema kweli wakati wote alikuwa akiwasiliana nasi, nakumbuka mtu wa kwanza kupiga kura alikuwa Raza (Mohamed, Mwakilishi wa Uzini) ambaye alikuwa Dubai na baada ya hapo alikwenda walikokuwa mahujaji wengine na walifanikisha vizuri sana,” alisema.

Wajumbe wengine waliokuwa Uarabuni kwa mujibu wa orodha iliyotangazwa na Mwenyekiti wa Bunge Maalumu, Samuel Sitta ni pamoja na Dk Abdallah Kigoda, Sheikh Mussa Kundecha, Hamza Mustapha Njozi, Dk Maua Daftari, Shawana Bukheti Hassan, Asha Mtwangi, Amina Andrew Clement na Riziki Lulida.

 

TEMBELEA MWANANCHI HAPA KUSOMA TAARIFA YOTE

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO