Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Meya wa Jiji la Arusha Kupitia CHADEMA Aja na Mikakati ya Jiji Kumiliki Timu Ligi Kuu


Mstahiki Meya wa Jiji la Arusha kupitia CHADEMA Mh Kalisti Lazaro akizindua Rasimu ya KATIBA ya ARUSHA CITY SPORTS CLUB, timu itakayomilikiwa na Jiji la Arusha.

Pamoja na uzinduzi huo wa rasimu, Mh Meya ameunda Kamati maalum ya wadau wa michezo itakayokuwa na jukumu la kutafuta timu iliyokwenye nafasi sahihi ya kununuliwa na Jiji la Arusha ili iweze kushiriki Ligi kuu Vodacom. 

Baadhi ya waheshimiwa madiwani, wadau wa michezo na watumishi wengine wa Halmashuri ya Jiji la Arusha katika picha ya pamoja na Mstahiki Meya Kalisti





Blogu hii inawatakia kila lakheri wana wa Arusha na uongozi wa Jiji kufanikiwa kuwa na timu ya Jiji katika Ligi Kuu ya Tanzania kwasababu michezo inaunganisha amii, michezo ni afya na michezo ni biashara/chazo cha mapato.


Picha: kwa hisani ya Diwani wa Levolosi, Ephata Nanyaro
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO