Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

BUNGE LAAHIRISHWA; VURUGU ZAIBUKA BAADA YA KUONEKANA MPANGO WA KUWANUSURU WATUHUMIWA WA ESCROW

Hali ya taharuki iliibuka ghafla Bungeni Ddodoma usiku huu    baada  ya  UKAWA na wabunge baadhi wa CCM kugoma  kuendelea  na  mjadala  wa  Bunge  wakishinikiza  Waziri  Muhongo  awajibishwe....

Hali hiyo ilitokea  baada  ya  kiongozi  wa  kambi  rasmi  ya  Upinzani  Bungeni, Mh. Freeman Mbowe  kusimama  na  kumtuhumu  Spika  wa Bunge kujaribu kuwakumbatia  wezi  wa  Pesa  za  Escrow, akijaribu kulazimisha mapendekezo ya Bunge kutokuwa na maneno ya kumtaka Rais awafukuze uwaziri, kwa wakati huo ilikuwa ni zamu ya Waziri Muhongo na badala yake iwe tu ushauri kwa Serikali iamuamue cha kuwafanya.
Spika alijaribu kumsihi Mh Mbowe aendelee kuzungumza lakini Mbowe akawa amesimama na wengine nao wakasimama na kuonekana wakipanga vitu vyao kama wanataka kutoka lakini hawakutoka na kuendelea kusimama wote.

Mh Ole sendeka akajaribu kuwasihi wakae ili kutafuta muafaka lakini haikuwezekana. Hatua hiyo  iliwafaya  wabunge  wa  upinzani  wasimame  na  kuanza  kuimba  nyimbo  za  kuwataka  wezi  watoke  ndani  ya  ukumbi  wa  Bunge. Na ndipo ikamlazimu  Spika  wa  Bunge  kuahirisha   Bunge  mpaka  watakapojadiliana.

 

Picha: Matukio na Vijana

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO