Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Wahuni wanaodaiwa kukodiwa na CCM wakiongozwa na Paul Makonda wavuruga mdahalo wa Katiba na kumpiga Jaji Warioba

Katika kile kinachoonekana kuwapo kwa hila ama jambo lisilo sawa katika Katiba inayopendekezwa, Jaji Mstaafu na aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Katiba amejikuta katika wakati mgumu na kudhalilishwa wakati wa mdahalo huru kuhusu maswala ya Katiba Mpya

Mdahao huo uliokuwa unarushwa live kupitia runinga ya ITV kutoka Ubungo Pearl ulikuwa na mada isemayo "Katiba Mpya-Maoni ya Wananchi na Katiba Inayopendekezwa" ulianza kwa amani na utulivu lakini ulikuka kuvurugika baada ya vijana wanaodaiwa kutumwa na viongozi wa CCM kuingilia kati na kuanzisha vurugu kubwa zilizopeleke mdahalo huo kuahirishwa.

Kiongozi wa UVCCM Paul Makonda analaumiwa kwa kuwa kinara wa vurugu hizo ambapo anadaiwa kuthubutu kumrushia chupa Jaji Warioba ambaye aliokolewa na wanausalama.

Wadadisi wa mambo wanatafsiri tukio hili la aibu kama sehemu ya muendelezo wa CCM kujaribu kuzuia ukweli mwingine kujilikana kuhusu Katiba Mpya ambayo yapaswa kuwa ni Katiba ya wananchi wote bila kubagua kundi lolote.

Itakumbukwa kuwa Katiba Inayopendekezwa imelazimishwa kupatikana kwa kukiuka baadhi ya taratibu na hata kufoji kura za maamuzi.

Picha hizi ni baadhi ya matukio wakati wa vurugu hizo.

 
 

 

 

 

ubungo pearl

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO