Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Rais Kikwete afanyiwa upasuaji tezidume

 Rais Kikwete afanyiwa upasuaji tezidume

RAIS Jakaya Kikwete, alfajiri ya juzi alifanyiwa upasuaji wa tezidume (prostrate), katika Hospitali ya Johns Hopkins iliyoko Baltimore, Jimbo la Maryland, Marekani.

Taarifa iliyotolewa na Ikulu kwa vyombo vya habari jana, ilisema kuwa Rais Kikwete amefanyiwa upasuaji huo baada ya madaktari waliomfanyia uchunguzi wa afya yake, kujiridhisha kuwa alikuwa anahitaji matibabu ya aina hiyo.

“Upasuaji huo uliofanyika alfajiri na kuchukua kiasi cha saa moja nusu, umefanyika salama na kwa mafanikio makubwa. Hali ya Mheshimiwa Rais Kikwete inaendelea vizuri, bado yuko wodini akiendelea kuwa chini ya uangalizi wa madaktari na kupatiwa tiba,” ilisema taarifa hiyo.

Aidha, taarifa hiyo pia iliwataka wananchi kuwa watulivu, kwani wataendelea kupewa taarifa sahihi kuhusu hali ya Rais Kikwete kwa kadri zitakavyokuwa zinapatikana.

Wiki iliyopita kupitia taarifa ya Ikulu kwa vyombo vya habari, ilisema kuwa aliondoka Jumatano na kwamba kulingana na ratiba ya uchunguzi wa afya yake angerejea nchini Alhamisi wiki hii.

Hata hivyo, taarifa hiyo iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, haikueleza bayana tatizo linalomsumbua Kikwete mbali ya kusisitiza kuwa amekwenda huko kwa ajili ya uchunguzi wa kitabibu.

Taarifa za hali ya afya ya Rais Kikwete kwa mara ya kwanza ziliwahi kutolewa mwaka 2009, muda mchache baada ya kushindwa kukamilisha hotuba aliyokuwa akiitoa kwenye sherehe za miaka 100 ya Kanisa la Africa Inland Church Tanzania (AICT), kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

CHANZO: Tanzania Daima

ANGALIA  ZA RAIS DK. J.K KIKWETE BAAADA NA KABLA YA KUFANYIWA UPASUAJI


Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO