Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

LEMA NA MUKYA TENA 2015; WAIBUKA KIDEDEA KURA ZA MAONI ARUSHA MJINI

SAM_3710

Mh Godbless Jonathan Lema akizungumza kwa furaha mara baada ya Msimamizi wa Uchaguzi wa Kura za Maoni Jimbo la Arusha Mjini (CHADEMA) ambaye pia ni Mbunge wa Rombo Mh Joseph Selasini kumtangaza kuwa mshindi kwa kupata kura 255 kati ya 274 ambazo ni sawa na 93.06% ya kura zote na kuwashinda Nsajigwa Mwakatobe aliyepata kura 6 (2.18% na Noel Olevaroya aliyejinyakulia kura 13 (4.74%). Kwa mara ya tatu Mh Lema anapata nafasi ya kugombea Ubunge Jimbo la Arusha Mjini. Mara ya kwanza ilikuwa mwaka 2005 na baadae mwaka 2010 aliposhinda na kuwa mbunge kabla ya kuvuliwa ubunge na Mahakama na kurudishiwa tena aliposhinda rufaa.

 SAM_3658

Lema akitumbukiza kura yake kwenye sanduku la kupigia kura

SAM_3716

Mtoto wa Lema akitoa salamu za shukrani kwa niaba ya baba yake kwa ushindi alioupata

SAM_3729

SAM_3686

Wakati wakisubiri matokeo yatangazwe

SAM_3660

SAM_3706

Joyce John Mukya akitoa salamu za shukrani kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Jimbo la Arusha Mjini na BAWACHA mara baada ya kutangazwa kinara wa wagombea ubunge Viti Maalumu kwa Jimbo la Arusha Mjini kwa asilimia 73.06 na kuwaacha mbali washindani wenzake saba.

SAM_3692

Tabasamu la furaha baada ya kufahamu ni mshindi

SAM_3690

Godbless Lema akisaini fomu za matokeo

SAM_3693

Joyce Mukya, mshindi wa kura za maoni Viti Maalumu akisaini fomu ya matokeo

SAM_3694

SAM_3697

Viola Likindikoki aliyekuwa anawania uteuzi wa Viti Maalumu nae pia akisaini fomu za mtokeo. Viola ni Mwenyekiti wa BAWACHA Wilaya ya Arusha Mjini

SAM_3699

Katibu wa Baraza la Vijana Arusha Mjini Mh Glory Kaaya aliyekuwa pia anawania nafasi ya Viti Maalumu kwa Jimbo la Arusha Mjini akisaini fomu ya matokeo

SAM_3703

Grace Macha akihutubia wajumbe na kuwashukuru kwa kura walizompatia japo hazikutosha kumtangaza mshindi

SAM_3628

Nsajigwa Mwakatobe akiomba kura kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu Jimbo la Arusha Mjini CHADEMA. Kura zake hazikutosha kumtangaza mshindi hata hivyo

SAM_3659

Wageni waalikwa wakifuatilia uchaguzi huo

SAM_3666

Bosi mzito wa Ausha255 “Noise of Silebce” akiteta jambo na mke wa Mh Lema Bi Neema Lema ukumbini hapo.

MATOKEO KAMILI HAYA HAPA
Ubunge Jimbo la Arusha Mjini
1. Godbless Lema- 255 (93.06%)2. Noel Olevaroya- 13 (4.74%)
3. Nsajigwa Mwakatobe - 6 (2.18%)
Jumla ya Kura - 274

Viti Maalumu Jimbo la Arusha Mjini
1. Viola Likindikoki - 5
2. Flora - 1
3. Theresa Minja - 1
4. Joyce Mukya - 39 (73.6%)
5. Grace Macha - 3
6. Pamela - 0
7. Glory Kaaya - 1
8. Prisca Massawe - 3

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO