Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Diwani pekee wa TLP Arusha avuliwa uanachama!

michael-kivuyoDiwani pekee wa kuchaguliwa wa chama cha Tanzania Labour Party (TLP),  Michael Kivuyo wa Kata ya Sokoni 1 Mkoani Arusha amevuliwa uanachama kwa kile kinachodaiwa kushindwa kusimamisha wagombea wa chama chake kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Jumapili kesho Disemba 14, 2014.

Uamuzi huo umechukuliwa na Kamati ya Utendaji ya TLP Wilaya ya Arusha Mjini baada ya kikao cha Sekretaieti ya chama hicho kuka Novemba 20 na kuamua hivyo.

Mwenyekiti wa TLP WIlaya ya Arusha Bw Deogratius Makishe akiongea na wanahabari alitangaza tuhuma tano kwa Kivuyo kuwa ni

1. Kushindwa kusimamisha wagombea wa Serikali za Mitaa

2. Kuhamasisha viongozi wa Serikali za Mitaa kwa tiketi ya TLP na kuwashawishi kugombea kupitia NCCR-Mageuzi

3. Kufanya kazi ya kuijenga NCCR –Mageuzi badala ya TLP 4 ambacho yeye ni Diwani wake

4. Kutotoa ushirikiano kwa viongozi wa TLP Wilaya na

5. Madai kwamba kwasasa Kivuyo ni mwanachama wa NCCR wakati ni Diwani kupitia TLP

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO