Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Mh Ester Matiko Afurahia Krismasi na Mamia ya Watoto Waishio Katika Mazingira Magumu Tarime na Kushuhudia Mpambano wa ESTER MATIKO CUP

Mbunge wa Viti Maalumu (CHADEMA) Mh Ester Matiko amesherehekea Siku Kuu ya Krismasi pamoja na watoto waishio katika mazingira magumu Tarime Mkoani Mara na kupata chakula pamoja kama sehemu ya Shukurani yake kwa Mungu kwa kumnusuru na ajali mbaya yeye na watoto wake majuma kadhaa yaliyopita.

Mh Matiko alijitolea ng’ombe, mchele kilo 100, soda maji na juice ambavyo ndivyo vilitumika kwa shughuli hiyo na watoto wakala na kunywa na kufurahia sikukuu

Sambamba na tukio hilo la chakula cha pamoja, kulikuwa na michezo mbalimbali kwa watoto hao kama kukimbia mbio fupi, kukimbiza kuku, kucheza muziki n.k na kuhitimishwa jioni na mechi kabambe ya mpira wa miguu baina ya MABOGI FC na MWEMA FC katika raundi ya nane ya michuano ya ESTER MATIKO FOOTBALL RISING CUP, vyote vikifanyikia katika uwanja wa Tarime.

Kwa michezo ya watoto wanaoishi katika mazigira magumu, washindi walipatiwa zawadi mbali mbali zikiwemo fedha taslimu kutoka kwa mbunge huyo.

Mh Ester Matiko, Mbunge Viti Maalumu (CHADEMA) akipatiwa chakula katika siku ya Krismasi, chakula alichoandaa kula pamoja kusherehekea sikukuu na watoto waishio katika mazingira magumu ndani ya mji wa Tarime na maeneo jirani

Mh Matiko akipata chakula na watoto wanaosishi katika mazingira magumu
 
Mh Ester Matiko akifafanua jambo kwa mmoja wa wadau walioambatana naye kwenye shughuli hiyo
 
Watoto wanaishi katika mazingira magumu wakijipatia chakula kilichoandaliwa na Mbunge Ester Matiko kusherehekea Sikukuu ya Krismas na watoto hao mjini Tarime
 
Waratibu wakiandikisha majina ya watoto wanashiriki michezo mbalimbali
 
Baadhi ya watoto waishio katika mazingira magumu Tarime wakiwa katika picha ya pamoja na Mbunge Ester Matiko
 
 
Baadhi ya watoto wakionesha ishara ya alama inayotumiwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo ambacho Mh Ester Matiko ni Mbunge anaetokana nacho.
Mh Matiko akioa neno la shukrani
Mmoja wa watoto waishia katika mazingira magumu akiondoka kutafuta mahali pa kukaa kula chakula
 
 
Mh Ester Matiko akitoa zawadi kwa baadhi ya washindi kwenye michezo ya watoto waishio katika mazingira magumu Tarime

Mechi kabambe baina ya Mabogi FC na Mwema FC ikiendelea katika raundi ya nane ya michuano ya ESTER MATIKO FOOTBALL RISING CUP. Mechi hiyo iliyanfyika jioni baada ya shughuli ya sikukuu na watoto uwanja wa Tarime ambapo Mwema FC waliwafunga Mabogi FC kwa jumla ya magoli 3 kwa 1.

PICHA ZOTE NA: ESTER MATIKO

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO