Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

KOREA YAKOSA INTERNET KWA MASAA 9, MAREKANI YAHISIWA KUHUSIKA!

Mawasiliano ya internet nchini Korea Kaskazini yamerejea leo Jumanne baada ya kupotea kwa zaidi ya saa tisa.

“Ni kama vile Korea Kaskazini ilifutwa kwenye ramani ya dunia ya Internet,” Rais wa kampuni ya masuala ya usalama iitwayo, CloudFlare, Matthew Prince aliiambia CNN.

Tatizo hilo limekuja wakati ambapo Korea Kaskazini na Marekani zipo kwenye vita vya maneno kufuatia kushambuliwa kimtandao kwa kampuni Sony Pictures. Marekani inaishutumu Korea Kaskazini kuwa imehusika japo yenyewe imekanusha.

Korea imechukizwa na filamu ya ‘The Interview’ inayosimulia kisasa cha kutunga cha mpango wa kuuawa kwa kiongozi wake, Kim Jong Un.

Kampuni ya Sony iliamua kusitisha kuizindua filamu hiyo kufuatia vitisho vya kigaidi kwenye majumba ya sinema.

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO