Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MASHINDANO YA WABUNGE EAC: BUNGE LA TANZANIA NA KENYA NGOMA DROO

 

SAM_0616

Wachezaji wa Tanzania na Kenya wakiwa katika mashindano ya wabunge wa jumuiya ya Afrika mashariki leo,  katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid Karume jijini Arusha, mechi hiyo ilivuta hisia za wakazi wa jiji hilo waliomiminika kuja kushuhudia wabunge hao wakimenyana uwanjani, baada ya dakika ya tano bunge la kenya walijipatia bao la kwanza, bao lililofungwa na Mh.Steven Nyatta na hatimaye Tanzania kusawazisha dakika ya 24 kwa njia ya penalt baada ya Mh.Mbunge Joshua Nassari kudondoshwa eneo la hatari kwa kugongwa na mlinda mlango wa kenya Kega Kanin.

SAM_0004Mbunge wa Jimbo la Kinondoni Mh Iddi Azan mlinda malango ambaye pia ni kiongozi wa timu ya bunge la Tanzania akinyaka magoli akionyesha umahiri wake wa kudaka mpira hali iliyosababisha mashabiki wa jiji la Arusha kumshangilia

SAM_0003Mlinda mlango wa Timu ya kenya Kega Kanin akijaribu kuzuia goli lililopatikana kwa njia ya penalt katika dakika ya 24

SAM_0018Naibu Waziri   wa  Fedha   Adam  Malima akichechemea uwanjani baada ya kuanguka na kupewa huduma ya kwanza

SAM_0613Muonekano jukwaa kuu

SAM_0012Wachezaji wa timu ya Tanzania wakijadiliana uwanjani kabla ya mechi kuanza

SAM_0013Wachezaji wa timu ya Kenya wakijadiliana uwanjani kabla ya mechi kuanza

SAM_0005Kushoto ni mchezaji wa timu ya kenya Mh.Peter Kaluma katikati ni Mh Dan Wanyama wa kenya mrefu kuliko wote uwanjani alipewa kadi nyekundu baada ya kuonekana akijibizana na mwamuzi aliyekuwa akichezesha mpambano huo kulia ni Mh Joshua Nassari wa Tanzania

SAM_0007Kushoto Mh Iddi Azan ambaye ni mlinda malango wa timu ya Tanzania akiwa katika mapumziko, aliyeshikilia mpira ni mwamuzi wa mpambano huo Erick OnokoSAM_0002Mh Joshua Nassari wa Tanzania akipewa huduma ya kwanza

SAM_0020Naibu Waziri   wa  Fedha   Adam  Malima akipatiwa huduma ya kwanza

SAM_0024Mh.Mbunge wa Tanzania akiwa amelala chali akionekana kuwa na maumivu makali baada ya kuumia katika mechi hiyo wabunge wenzake wakijaribu kumsaidiaSAM_0006Mashabiki wa Kenya wakiwa wanashangilia huku wakiwa wanaonyesha bwebweeee zao

SAM_0614Umati wa watu waliokuja kushuhudia mpambano wa Tanzania na Kenya

SAM_0014Mashabiki wa Tanzania wakiwa wanashangilia kwa kuzunguka uwanja

SAM_0615Watoa huduma ya kwanza kutoka msalaba mwekundu wakiwa wanafatilia mechi ya wabunge wa Afrika mashariki

 

eac 

 

WAKATI HUO HUO.. PAMELLA MOLEL ANARIPOTI KWAMBA

TIMU YA EALA IMEICHAPA BURUNDI 4-2

SAM_0035

(Wachezaji wa Timu ya EALA waliovalia jezi rangi ya blue wakipambana na wenzao timu ya Burundi)

Timu ya wabunge wa EALA wameicharaza mabao manne kwa mbili timu ya Burundi jana katika Uwanja Sheikh Amri Abeid  jijini Arusha ikiwa ni muendelezo wa mashindano ya wabunge Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)

Mchezaji mahiri wa timu ya Eala John King aliipatia mabao 3 timu yake dakika ya 9 na 21 kipindi cha kwanza hali iliyosabaisha mashabiki waliomiminika katika uwanja huo kumshangila

Kipindi cha pili hali ilibadilika  baada ya timu ya Burundi kujipatia mabao mawili  dakika ya nne na dakika ya 18, mpigaji wa magoli hayo ni Simon Gahinja

Baada ya mchuano mkali wa timu zote mbili ,Eala waliongeza bao la 4 lililofungwa na mchezaji Wilyclif Keto dakika ya 25 baada ya kupata penalt dakika 33  ambapo mpigaji penalt alikosa baada ya mlinda mlango wa Burundi Ibrahim Uwizey kudaka

SAM_0039Mbunge wa EALA kutoka nchini Tanzania Mh.Twaha Taslama jezi namba 12 akiwa uwanjani

SAM_0038

Mh Mbunge wa Eala Bernad Mrunya akiwa anajiandaa kukabilia na timu ya Burundi katika Uwanja Sheikh Amri Abeid  jijini Arusha ikiwa ni muendelezo wa mashindano ya wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO