Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Simanzi: Mgombea Ubunge Arusha Mjini kupitia ACT Wazalendo, Estomih Mallah Afariki Hospitalini KCMC Moshi

By Louis Kolumbia, Mwananchi Digital

estomihMgombea Ubunge kupitia ACT-Wazalendo Jimbo la Arusha Mjini amafariki dunia katika hospitali ya Kilimanjaro Christian Medical Center (KCMC) usiku wa kuamkia leo .

Makamu mwenyekiti wa ACT-Wazalendo , Shaaban Mambo amezungumza na  Mwananchi Digital kwa amepokea simu kutoka kwa mtoto wa marehemu mapema leo asubuhi akimueleza kuwa baba yao amefariki.

Taarifa za awali zinaeleza kuwa Bw Mallah alijisikia kuumwa siku ya Jumanne Tuesday mara baada ya mkutano wa kampeni za mgombea Urais wa chama hicho Anna Mghwira maeneo ya Ngaramtoni. Akapelekwa hospitali ya  St. Thomas Hospital iliyopo Jijini Arusha ambao alikuwa akitibiwa hadi jana alipohamishiwa  KCMC kwa matibabu zaidi.

Mipango ya mazishi inaendelea na taarifa itatolewa baada ya kikao cha familia.

Kwa mujibu wa Bw. Mambo, Mallah, aliyekuwa akiongoza Kamati ya fedha ya chama hicho, alikuwa na mchango mkubwa katika ukuaji wa ACT Wazalendo na kwamba chama kimempoteza mtu muhimu sana.

Mwaka  2010, alishinda kiti cha Udiwani Kata ya  Kimandolu Ward kupitia CHADEMA. mapema mwaka 2011, Mallah na madiwani wengine watatu wa CHADEMA (John Bayo (Elerai), Reuben Ngowi (Themi) na Charles Mpanda (Kaloleni) walivuliwa uanachama  wao katika mgogoro baina ya CCM na Chadema kuhusiana na kilichodaiwa kuwa uchaguzi batili wa meya wa Jiji.

Baadae Bw Mallah akajiunga na ACT-Wazalendo ambapo alipata nafasi ya kuwakilisha chama hicho katika kinyang’anyiro cha Ubunge Arusha Mjini katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe Oktoba 25 mwaka huu, na kupambana na Mbunge anayemaliza muda wake MP Godbless Lema (Chadema). Mshindani mwingine wa Karibu kwa lema ni Bw Philemon Mollel (CCM).

SOURCE: THE CITIZEN

BLOGU HII INAWAPA POLE WAFIWA WOTE HASA, FAMILIA NA CHAMA CHAKE NA MUNGU AIWEKE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA. AMINA!

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO