Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Mama Samia Suluhu Awasili Kigoma, Wananchi Wasimamisha Shughuli Kumlaki


Baadhi ya wananchi na wanaCCM wakiwa wamemsimamisha mgombea mwenza wa CCM nafasi ya urais, Mama Samia Suluhu Hassan Kata ya Igagala, Uvinza Mkoani Kigoma wakimtaka awasalimie kabla ya kuendelea na safari. Mgombea mwenza huyo wa CCM ameingia mkoani Kigoma kwa ziara ya kampeni kuinadi ilani ya CCM.

Baadhi ya Wananchi wakiwa wamesimama pemezoni mwa barabara kumlaki mgombea mwenza wa urais CCM alipokuwa akiwasili Mkoani Kigoma kufanya mikutano yake ya kampeni.

Mgombea mwenza akizungumza na wananchi waliomsimamisha njiani kuwasilisha kero zao.
Mgombea mwenza CCM, Mama Suluhu akiwa ameshikilia kadi na bendera za vyama vya upinzani alizokabidhiwa na vijana waliohama vyama vyao na kujiunga na CCM, alipokuwa akiwasili Mkoani Kigoma mwisho wa reli.
Baadhi ya wananchi na wanaCCM wakiwa wamemsimamisha mgombea mwenza wa CCM nafasi ya urais, Mama Samia Suluhu Hassan Kijiji cha Mlyabibi, Mkoani Kigoma wakimtaka awasalimie kabla ya kuendelea na safari. Mgombea mwenza huyo wa CCM ameingia mkoani Kigoma kwa ziara ya kampeni kuinadi ilani ya CCM.
Wananchi na wanaCCM wakimshangilia mgombea mwenza wa CCM, Mama Samia Suluhu Hassan alipokuwa akiwasili mkoani Kigoma kuanza ziara yake ya kampeni. Mama Suluhu kawasili mkoani Kigoma na kufanya mikutano ya kampeni katika majimbo ya Kigoma Kusini, Kigoma Kaskazini na Kigoma Mjini.
Mgombea mwenza wa CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akiwasili Uwanja wa Tarafa Mwandika mkoani Kigoma kuhutubia wananchi katika ziara yake ya kampeni mkoani humo.
Baadhi ya vijana waliohama kutoka chama cha NCCR-Mageuzi na kujiunga na CCM wakiwa wamemnyanyua juu mmoja wa viongozi aliyewashawishi kujiunga na chama hicho mara baada ya kupokelewa na mgombea mwenza wa CCM kwenye mkutano wa kampeni mjini Uvinza Kigoma. Zaidi ya vijana 60 wakiongozwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa chama cha NCCR-Kata ya Uvinza, Himid Kisobwe wamejiunga na CCM na kupokelewa na Mama Samia Suluhu.
Vijana waliojiunga na CCM kutokea chama cha NCCR-Mageuzi wakishangilia mara baada ya kumpokea Mama Samia Suluhu katika mkutano wa hadhara. Zaidi ya vijana 60 wakiongozwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa chama cha NCCR-Kata ya Uvinza, Himid Kisobwe wamejiunga na CCM na kupokelewa na Mama Samia Suluhu.
Mgombea mwenza wa CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akiwasili Uwanja wa Tarafa Mwandika mkoani Kigoma kuhutubia wananchi katika ziara yake ya kampeni mkoani humo.
Mgombea mwenza wa CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akifurahia jambo katika mkutano wa kampeni uliofanyika Uwanja wa Community Center Jimbo la Kigoma Mjini.
Burudani baada ya mapokezi ya mgombea mwenza kuwasili mkoani Kigoma.
Mgombea ubunge Jimbo la Kigoma Kaskazini, Peter Serukamba (kulia) akisalimiana na mgombea mwenza wa CCM, Mama Samia Suluhu Hassan alipowasili Uwanja wa Tarafa Mwandika mkoani Kigoma kuhutubia wananchi katika ziara yake ya kampeni mkoani humo.
Mgombea ubunge Jimbo la Kigoma Kaskazini, Peter Serukamba akizungumza na wananchi katika mkutano huo.
Mgombea mwenza wa CCM, Mama Samia Suluhu Hassan (hayupo pichani) akiwahutubia wanaCCM na wananchi katika Uwanja wa Community Center Jimbo la Kigoma Mjini.

Mgombea mwenza wa CCM, Mama Samia Suluhu Hassan (hayupo pichani) akiwahutubia wanaCCM na wananchi katika Uwanja wa Community Center Jimbo la Kigoma Mjini. Picha na www.thehabari.com/Kigoma.

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO