Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

RAIS KIKWETE ATUNUKU NISHANI ZA MIAKA 50 YA JWTZ

Rais Jakaya Kikwete akimtunuku nishani ya kumbukumbu ya miaka 50 ya Jeshi la Wanachi wa Tanzania JWTZ, Mkuu wa majeshi ya Ulinzi nchini, Jenerali Davis Mwamunyange katika sherehe za kutunuku nishani zilizofanyika kwenye ukumbi wa Jenerali Kiwelu wa Chuo cha Mafunzo ya Maafisa wa Jeshi Tanzania, Monduli, Septemba 6, 2014.

Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na maofisa wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ baada ya kuwatunuku nishani katika sherehe zilizofanyika kwenye ukumbi wa Jenerali Kiwelu wa Chuo cha Mafunzo ya Maafisa wa Jeshi Tanzania, Monduli, Septemba 6, 2014. Kulia kwake ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini, Jeneral Davis Mwamunyange.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue katika sherehe za kutunuku nishani zilizofanyika kwenye ukumbi wa Jenerali Kiwelu wa Chuo cha Mafunzo ya Maafisa wa Jeshi Tanzania, Monduli, Septemba 6, 2014.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiagana na maofisa wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ baada ya Rais Jakaya Kikwete kutunuku nishani katika sherehe zilizofanyika kwenye ukumbi wa Jenerali Kiwelu wa Chuo cha Mafunzo ya Maafisa wa Jeshi Tanzania, Monduli, Septemba 6, 2014. Kushoto ni Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa na wapili kushoto ni waziri Mkuu Mstaafu John Malecela.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO