Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MH. CATHERINE MAGIGE AZINDUA DUKA JIPYA LA UREMBO LA ZuRii LILILOPO DAR FREE MARKET

magige

DSC_0312

Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Arusha, Catherine Magige (kushoto) akiwasili kuzindua rasmi duka la urembo la ZuRii House of Beauty linalomilikiwa na mwana Diaspora ambaye pia ni mwanalibeneke Jestina George Meru (kulia) ndani ya jengo la Dar Free Market jijini Dar es Salaam jana.

Na Mwandishi  Wetu

Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Arusha, Catherine Magige leo amezindua rasmi  rasmi duka  jipya la vipodozi na vitu mbalimbali linalofahamika kwa jina la ZuRii lililopo katika jengo la Dar Free Market lililopo katika barabara ya Alli Hassan Mwinyi  Jijini Dar es Salaam.

Akizindua duka hilo ambalo linamilikiwa na mwana Diaspora ambaye pia ni mwanalibeneke Jestina George, Magige alisema kwamba amevutiwa na namna Jestina alivyoweza kurudi na kuwekeza  nyumbani hali ambayo imeweza kuzalisha ajira kwa watanzania na kuwa mfano wa kuigwa.

“Kabla ya yote nachukua fursa hii kumpongeza  Jestina  kwani ameonesha  mfano  wa umuhimu wa kujiajiri hasa kwa wanawake pia huu ni mfano wa kuigwa  kwa wanadiaspora , wengine warudi na kuja kuwekeza nyumbani kwani fursa nyingi zipo hivyo waje wazitumie” alisema Magige.

DSC_0214

Michuzi Media Group ikiongozwa Ahmad Michuzi mwanalibeneke wa Michuzijr Blog ( wa pili kulia) akiwa ameongozana na Mwanalibeneke wa Fullshwangwe Blog John Bukuku wakiwasili kwenye uzinduzi huo.

Aidha alitoa rai kwa wanawake wengine hapa nchini ambao wanauwezo wa kuwa na mitaji ya kuanzisha biashara wajiajiri na kutoa ajira kwa wengine  pia natoa wito kwa watanzania wengine waje katika duka la ZuRii kuja kutoa sapoti kwa Jestina, alisema Magige.

Wakati huohuo mmiliki wa duka hilo la ZuRii Jestina alisema kwamba yeye ameona  fursa za  kuwekeza nyumbani  hivyo ameamua kuzitumia ipasavyo.

“Natoa wito kwa kwa wanadiaspora wenzangu ni kwamba wasiwe na tabia za kuja likizo nyumbani nakuinjoi tu  fedha zao tu bali wajitahidi kuja kuwekeza kwani fursa zipo, kuanzisha duka hili ni ndoto yangu ya siku nyingi hivyo haya ni matokeo ya njozi yangu namshukuru  Mungu kwa kutimiza ndoto hii”.    

DSC_0317

Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Arusha, Mh. Catherine Magige akikata utepe kuzindua rasmi duka la ZuRii House of Beauty linalomilikiwa na Mwana Diaspora ambaye pia ni Blogger Jestina George Meru (anayeshuhudia tukio hilo).

DSC_0324

Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Arusha, Mh. Catherine Magige akiingia ndani ya duka hilo mara baada ya kulizindua.

DSC_0262

Mmiliki wa duka la urembo la ZuRii House of Beauty na mwana Diaspora ambaye pia ni mwanalibeneke Jestina George Meru akitoa maelezo ya baadhi ya bidhaa zake za urembo ambazo ni original kutoka nchini Uingereza na Marekani kwa Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Arusha, Mh. Catherine Magige.

DSC_0283

DSC_0264

DSC_0303

Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Arusha, Mh. Catherine Magige akiangalia bidhaa za urembo wa nywele ndani ya dula la ZuRii House of Beauty lililopo ndani ya jengo la Dar Free Market linalomilikiwa na Mwana Diaspora Jestina George Meru.

DSC_0296

Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Arusha, Mh. Catherine Magige akikagua moja ya bidhaa za nywele ndani ya duka hilo.

DSC_0231

Mmiliki wa duka la urembo la ZuRii House of Beauty na mwana Diaspora ambaye pia ni mwanalibeneke Jestina George Meru akitoa ushauri na maelezo kwa baadhi ya wateja waliofika dukani kwake mara baada ya kuzinduliwa rasmi jana jijini Dar.

DSC_0164

Raia wa kigeni nao walivutiwa na bidhaa za duka la ZuRii House of Beauty.

DSC_0170

Mwanalibeneke Khadija Khalili akiangalia baadhi ya bidhaa ndani ya duka ZuRii House of Beauty.

DSC_0193

Wateja wakiendelea kumiminika na kujichagulia bidhaa mbalimbali vikiwemo vibanio vya nywele vya wakubwa kwa watoto ndani ya duka ZuRii House of Beauty.

DSC_0228

DSC_0339

Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Arusha, Mh. Catherine Magige akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) waliohudhuria uzinduzi huo uliofanyika jana jijini Dar es Salaam.

DSC_0337

Mmiliki wa duka la urembo la ZuRii House of Beauty na mwana Diaspora ambaye pia ni mwanalibeneke Jestina George Meru akimpa mkono wa shukrani ya kubariki uzinduzi duka hilo Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Arusha, Mh. Catherine Magige jana jijini Dar es Salaam.

Mmiliki wa Duka la Zurii, Jestina George katika akizungumza na wanahabari katika uzinduzi wa duka hilo leo.
Mmiliki wa Duka la Zurii, Jestina George katika akizungumza na wanahabari katika uzinduzi wa duka hilo jana.
Baadhi ya wamiliki wa mitandao ya kijamii pamoja na waendeshaji wa mitandao hiyo wakiwa katika picha ya pamoja  katika uzinduzi wa duka hilo.
Baadhi ya wamiliki wa mitandao ya kijamii pamoja na waendeshaji wa mitandao hiyo wakiwa katika picha ya pamoja katika uzinduzi wa duka hilo.
Jestina George kulia akizungumza na baadhi ya wanabloggers katika uzinduzi wa duka hilo leo.
Jestina George kulia akizungumza na baadhi ya wanabloggers katika uzinduzi wa duka hilo jana.
Baadhi ya wamiliki wa mitandao ya kijamii pamoja na waendeshaji wa mitandao hiyo wakiwa katika picha ya pamoja  katika uzinduzi wa duka hilo.
Baadhi ya wamiliki wa mitandao ya kijamii pamoja na waendeshaji wa mitandao hiyo wakiwa katika picha ya pamoja katika uzinduzi wa duka hilo.
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO