Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

“Mgomo” wa Daladala Arusha Waingia Siku ya Pili kwa Baadhi ya Njia, Wasafiri Walazimika Kupanda Guta, Pick Up na Canter Kwenda Kazini

Kile kinachotafsiriwa kuwa mgomo wa waendesha magari madogo ya kubeba abiria kwa Jiji la Arusha maarufu kama “vifodi” umeendelea tena hii leo ikiwa ni siku ya pili mfululizo kwa baadhi ya njia. Kwa mfano kwa njia ya kutoka maeneo ya Moshono kuelekea mjini hakuna gari yeyete ya abiria kabisa, halikadhalika njia itokayo Njiro kwenye mjini pia.

Wasafiri wa njia hizo wamejikuta wakilazimika kusafiri katika mazingira ya hatari kwa kujazana kwenye magari ya wazi na pikipiki za mizigo vyombo ambavyo si maalumu kwa ubebeaji wa abiria.

Uchunguzi wa Blog hii umegundua kuwa wanaosababisha zaidi hali hii ni wapiga debe ambao wanaona kwa mfumo mpya wa hizi njia za usafiri kama mpango wa Jiji kukabiliana na msongamano barabarani hawataweza kupata ujira wa kuitia abiria kwenye magari, na hivyo baadhi yao kuwafanyia vurugu madereva wanaotaka kufanya kazi. Lakini pia kuna baadhi ya madereva ambao ni kama hawauelewa utaratibu huo mpya na kujikuta wakigoma kuendesha magari yao.

Picha zifuatazo zinasimualia baadhi ya matukio barabarani.

10945926_10206209432461067_618369046_n

10945148_10206209432101058_86714147_n

10942264_10206209425620896_109277478_nWanafunzi wakilazimika kutembea kwa miguu kuelekea shuleni

10934633_10206209425380890_1698646785_n

10934354_10206209417460692_719586644_n

10943120_10206209417660697_2019217090_n

10943166_10206209478102208_404477145_n

10917757_10206209432741074_1219896982_n

10847140_10206209478702223_1921904825_n

10721199_10206209649306488_50490285_n

10945951_10206209649586495_1359633223_n

1601570_328703774003994_7699176808893976460_n

10947226_328703570670681_4548256768399426743_n

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO