Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Chadema Arusha Mjini Waanza Kuwafunda Wenyeviti Wao Wa Serikali za Mitaa

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Jimbo la Arusha Mjini kimeanza hii leo kuendesha semina za kuwapa muongozo wa kiutendaji kama viongozi wapya wa chama hicho, Wenyeviti na Wajumbe wao walioshinda kuongoza Serikali za Mitaa kupitia chama hicho.

Mafunzo hayo yameanza rasmi hii leo katika hotel ya kitalii ya New Arusha ya Jijini hapa na yanatarajiwa kuendelea tena kesho.

Chadema ilishinda jumla ya mitaa 76 kati ya 155 iliyoorodheshwa kufanya chaguzi na kati ya hiyo mitaa mitano haikuwa na uchaguzi baada ya wagombe wa Chadema kuenguliwa kwa sababu mbalimbali na kuachia wagombea wa CCM kupita bila kupingwa.

Aidha Chadema ina mitaa 5 ambayo wajumbe wote wa Serikali wanatokana nayo lakini wenyeviti ni wa CCM ambayo ilishinda mitaa 73 na hiyo mitano bila kupingwa.

Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na Chadema, Chadema wanaumiliki wa mabaraza ya maamuzi katika Kata 11

DSC00968

DSC00970

Mbunge wa Arusha Mjini Mh Godbless Lema (CHADEMA) akizungumza katika semina hiyo

DSC00974

Baadhi ya wenyeii na wajumbe wa Serikali za Mitaa watokanao na CHADEMA katika Jiji la Arusha wakisikiliza semina kwa makini

DSC00978

Mtoa mada Innocent Kisanyage akionekana kufafanua jambo wakati wa semina hiyo

 
 
Viongozi wa mabaraza ya Chadema. Kutoka Kushoto ni Mwenyekiti wa Baraza la Wazee maarufu kama “Baba Boni” anafuatiwa na Katibu wa Baraza la Wanawake ambaye pia ni Diwani wa Viti Maalumu Lemara, Diwani Viola pamoja na Mwenyekiti wake wa Baraza hili kwa Wilaya ya Arusha Mjini wakipitia Katiba ya hama chao
 
Mwanamama Sara Jonas ambaye ni mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Moshono Kaskazini
 
 
 
Wanasemina wakiwa makini kurekodi mambo muhimu
Katibu wa Chadema WIlaya ya Arusha Mjini, Bw Lewis Kopwe akitoa nasaa kamabla ya kuanza semina husika.
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO