Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Madiwani wa Manispaa ya Moshi Wagoma Kupitisha Bajeti ya Halmashauri Wakishinikiza Mkurugenzi Arudishe Kiwanja Cha Umma Alichomilikishwa Mtu Binafsi

Taarifa kutoka Manispaa ya Moshi zilizoifikia Blog hii muda huu zinaeleza kuwa Kikao cha Bajeti ya Hamlashauri hiyo kimeshindwa kuamua haima ya bajeti husika mapema leo asubuhi baada ya Madiwani walio wengi wa Chadema wakiongozwa na Meya Jaffari kugomea kupitisha bajeti hiyo kwa madai kwamba Mkurugenzi wa Hamlashauri hiyo anatakiwa arudishe kwanza kiwanja cha umma (open space) anayodaiwa kushiriki kummilikisha kwa mtu binafsi.

Mkurugenzi huyo Bw Shabani Ntarambe anadaiwa kumuagiza afisa mipango miji wa Manispaa hiyo kuandaa hati ya umiliki wa kiwanja kilichoelezwa kuwa cha umma kwa mtu binafsi (Mawenzi SPort Club). Kiwanja hicho ni eneo lililopo jirani na Kituo Kikuu cha Polisi ambako ndipo zilipo Osifi za Kata na Tarafa ya Mawenzi na viongozi wote wa Kata na Tarafa wanaitumia ofisi hiyo.

Kwa mujibu wa maelezo ya Diwani Hawa Ali wa Manispaa hiyo, inadaiwa kuwa walifanya uchunguzi baada ya kupata tetesi za mpango wa kugawa eneo hilo kwa mtu binafsi na wakaweka kizuizi lakini baadae wakagundua kuwa Mkurugenzi amamuagiza mwanasheria kuondoa zuio hilo na hatimaye mtu huyo aliyemilikishwa “Mawenzi Sport Club” kupatiwa hati ya umiliki jana. na kwamba ni kiwanja ambacho kilishatangazwa kama eneo la uwekezaji.

Blog hii inaendelea kufuatilia sakata hilo na kukujuza zaidi mauziano hayo yalikuwaje na mmiliki halali hasa ni nani!

 

IMG-20150121-WA0025

Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa a Moshi Mjini wakitoka nje ya Ukumbi wa Mkutano baada ya kugoma kuitisha bajeti hiyo hii leo asubuhi

IMG-20150121-WA0026
Meya wa Manispaa ya Moshi, Diwani Jaffari

IMG-20150121-WA0027

Madiwani na wanahabari wakiwa nje ya lango la Ofisi ya Manispaa ya Moshi

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO