Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Ratiba ya Mikutano ya Shukrani ya Chadema Jijini Arusha Hii Hapa!

lema na wananchi

Picha ya Makataba: Mbunge wa Arusha Mjini, Mh, Godbless Lema akihutubia wananchi katika moja ya mikutano ya chama chake Chadema Jijini Arusha.
*****

Katibu wa Chadema Jimbo la Arusha Mjini, Bw Lewis Kopwe na Katibu Mwenezi wake Bw Gabriel Kivuyo wametoa ratiba ya mikutano mfululizo ya chama hicho kwa Kata kadhaa za Jimbo la Arusha Mjini zikilenga kuwakutanisha wananchi na viongozi wapya waliowachagua kuongoza Serikali za Mitaa maeneo tofauti ya Jiji.

Ratiba hiyo ni kama ifuatavyo

No.
Tarehe
Eneo la Mkutano/Mtaa
Kata
Maelezo
01 05/01/2015 Samunge Levolosi Umeshafanyika
02 10/01/2015 Shuma Elerai
03 17/01/2015 Esso Unga Ltd
04 24/01/2015 FFU Murriet
05 31/01/2015 Soko Kuu Kati
06 05/02/2015 Kambi ya Fisi Ngarenaro
07 07/02/2015 Bluehouse Daraja Mbili


Aidha Katibu huyo amesema kuwa kutakuwa na mikutano ya ziada nje na ratiba hii kwa maeneo mengine kuanzia tarehe 18/01/2015 mfululizo hadi tarehe 24/01/2015 ambapo baadhi ya wabunge wa chama hicho wamealikwa na viongozi wa Kata nyingine kuzungumza na wananchi.

Mwenyekiti wa chama hicho Jimbo la Arusha Mjini, Bw Derick Magoma amethibitisha kuwa mikutano hii yote na ratiba yake kama ilivyo tayari ina baraka za Jeshi la Polisi kuhakikisha wanatoa ulinzi maeneo hayo.

Ikumbukwe kuwa katika uchaguzi ulioisha Chadema wameshinda jumla ya mitaa 76 kwa wenyeviti wa wajumbe wote na mitaa 5 wakiwa na wajumbe wote wao isipokuwa Mwenyekiti!

CCM wao wameshinda mitaa 78 ueyekiti lakini katika hiyo mitaa mitano wajumbe wote ni wa Chadema na mitaa 6 haikuwa na ushindani baada ya wagombea wa Chadema kuenguliwa. Kwa hiyo ni sawa na kusema katika mitaa ambayo wameshindana CCM imepata Mitaa 67 pekee ikiwa ni matokeo ya mbinu ovu na hila za kila namna pamoja na msaada wa wasimamizi na polisi.

 

CHANZO: JAMII FORUMS

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO