Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

TAKUKURU YACHUNGUZA UFISADI CARMATEC ARUSHA

 

carmatec


Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(Takukuru) mkoani Arusha imemhoji mkurugenzi mkuu wa kituo cha zana za kilimo na teknolojia vijijini (Carmatec),Elfariji Makongoro pamoja na baadhi ya watumishi wa taasisi hiyo kutokana na sakata la ufisadi wa majengo mawili makubwa yaliyopo ndani ya taasisi hiyo.


Majengo hayo ni yale yanayotazamana mkabala na kiwanda cha kutengeneza matairi cha General Tyre cha jijini Arusha ambapo taasisi hiyo iliyafungulia zabuni  mwaka jana kwa ajili ya kuyapangisha mwaka juzi lakini katika hali isiyo ya kawaida mara baada ya kutangaza kwa washindi wa zabuni hizo na malipo kufanyika mchakato huo ulisitishwa ghafla.


Hadi sasa majengo hayo yako wazi kufuatia washindi wa zabuni hizo kufungua shauri lao mahakamani wakitaka kulipwa fedha walizolipa kwa ajili ya kupangisha ndani ya majengo hayo ambazo ni zaidi ya $ 10,000 sawa na zaidi ya sh,15 milioni.

 

Habari na:  Moses Mashalla

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO