Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

TASWIRA KATIKA KIKAKO CHA BARAZA LA UONGOZI WA KANDA YA KASKAZINI -KATIKA HOTELI YA THE NEW ARUSHA HOTEL

 

Mwenyekiti wa Chadema Taifa Mhe Freeman A.Mbowe akiwa ameambatana na Mwenyekiti wa Kanda ya Kaskazini Mhe Israel Natse wakiwa wanaingia ukumbi wa JUMUIKA

Viongozi wa kuu wa Chadema Taifa pamoja na Kanda wakiimba wimbo wa Taifa kabla ya kikao cha baraza la kanda ya kaskazini kuanza

Waheshimiwa wabunge wakiwa wanaimba wimbo wa Taifa

Katibu wa Kanda ya kaskazini Mhe Amani Golugwa akiwakaribisha wajumbe wa kikao cha baraza la Kanda ya Kaskazini , wajumbe wa kikao wametoka katika majimbo 33 ya kanda


Mwenyekiti wa Kanda ya kaskazini Mhe Israel Nates akitoa neno la ufunguzi kwa wajumbe na kumkaribisha Naibu katibu Mkuu Zanzibar

Naibu katibu Mkuu Zanzibar Mhe Salimu Mwalimu akiongea na Wajumbe wa baraza la uongozi wa kanda ,na kufafanua majukumu na utekelezaji wa kanda kaitika ujenzi wa chama

Mhe Freeman A.Mbowe akiwa hutubia wajumbe wa baraza la kanda pamoja na waandishi wa habari, akifafanua baadhi ya mambo ambayo yanaendendea katika nchi yetu kwa sasa, pia akiitaka tume kuwa na msimamo wa siku na tarehe ya kuanza zoezi la uandikishaji wa Wanachi kwenye daftari la kupiga kura

Mwenyekiti huyo amesema kuwa  chama chao kimejipanga kuahakikisha kinahamasisha  kwa  nguvu zote wananchi weweze kwenda kujiandikisha katika  daftari la mpiga kura

Alisemakuwa hii itaweza kumsaidia kila mwananchi  kuweza kupata haki yakumchagua kiongozi bora  anaemtaka  katika uchaguzi mkuu  ujao  wa kuwachagua viongozi wakuu ambao ni rais ,wabunge na madiwani.

Alisema kuwa pamoja ya kuwa tume wamekuwa wananchelewesha kufanyika kwa zoezi hili , wao wamejipanga kikamilifu na pindi ambapo zoezi hili litatangazwa  kuanza rasmi watajitaidi kwa njia yoyote kuhamasisha wananchi wajitokeze kwa wingi kujiandikisha

Alisema kuwa kwa upande wa kupiga kura katiba wanaendelea na msimamo wao ambao walitangaza awali wa kutoshiriki katika mchakato wa kura ya maoni ya katiba  huku akisisitiza kuwa swala la kutoshiriki katika mchakato wakura za maoni auingiliani kabisa na  kuhamasisha wananchi kujiandikisha katika daftari la kudumu la mpiga kura 

Alimaliizia kwa kuwasihi wananchi wajitokeze kwa wingi  sana pindi pale ambapo watasikia zoezi la kujiandikisha kwenye daftari la kudumu limewadia  ili waweze kupata haki yao ambayo itawaruhusu kuchgua kiongozi wanao wataka.

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO