Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

DK. KIGWANGALLA ATUNUKU VYETI WAHITIMU SEKTA YA MAENDELEO YA JAMII TENGERU

 
Serikali inajipanga kwajili wataalamu wa maendeleo ya jamii 5,554 kwa kipindi cha miaka mitano ili waweze kutoa huduma za maendeleo ya jamii kuanzia  ngazi ya Serikali kuu hadi kijiji kama ilivyokuwa kwa utawala wa awamu ya kwanza nchini.
 
Ameyasema hayo katika Mahafali ya sita ya Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tenguru nje kidogo ya jiji  la Arusha Naibu Waziri Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Hamis Kigwangalla amesema serikali ya awamu ya kwanza ilikuwa na idadi kubwa ya mabibi na mabwana maendeleo ya jamii kila kata.
 Aliongeza kuwa kwasasa wataalamu katika sekta ya maendeleo ya jamii  wameanza kupungua sana na kukitaka chuo kuongeza udaili wa wanafunzi ili kuendana na azima ya serikali ya kuwa na wataalamu awa kila wilaya na kata.
 

Aidha aliitaka Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru kuendela kutoa taaluma yenye viwango na  bora na uzingatiwe katika mchakato wote wa utoaji mafunzo kuanzia kwenye udahili wa wanafunzi wenye sifa na vigezo ili kujenga jamii ya wasomi wenye tija katika Taifa letu

CHANZO: VERO IGNATUS
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO