Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Soma Hapa Orodha ya vyuo 26 vilivyofutiwa usajili na NACTE leo


Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) limevifungia vyuo vya ufundi 26 kutokana na makosa mbalimbali, ikiwamo kushindwa kuzingatia masharti yaliyowekwa katika cheti cha usajili wa vyuo hivyo, huku likisimamsisha utoaji wa programu zilizokuwa zikitolewa katika vyuo 20 ambazo hazijasajiliwa.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, Kaimu Katibu mtendaji wa NACTE, Dkt. Adolf Rutayuga, alisema kuwa wamekuwa wakifuatilia vyuo vya ufundi ili kutathmini kama vinafuata viwango vya ubora wa kitaaluma vilivyowekwa na NACTE katika kutoa mafunzo.
Katibu huyo amesema kuwa baada ya kufanya uchunguzi huo, wamebaini vyuo 26 vilishindwa kuzingatia masharti yaliyowekwa na NACTE katika cheti cha usajili, huku vyuo 20 vikitoa mafunzo ambayo hayajathibitishwa chini ya idara isiyotambulika,wakati vyuo viwili vikiwa na vituo vya satellite/Kampasi ambavyo navyo havijathibitishwa na chombo husika.

NACTE ni bodi iliyoanzishwa kisheria chini ya Sheria ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi, kifungu cha 129, kusimamia na kuratibu utoaji wa elimu ya ufundi na mafunzo nchini Tanzania.  Chini ya sheria hiyo, ili kufikia na kudumisha hali ya mtoa mafunzo, vyuo vyote vinatakiwa viwe vimesajiliwa, vibali na kuwa mitaala iliyopitishwa na baraza. Vyuo haviruhusiwi kuanza kutoa kuanza kutoa huduma yoyote ya mafunzo bila idhini ya baraza.
Hapa chini ni mgwanyo wa vyuo katika makundi matatu na hatua zilizochokuliwa dhidi ya kila kundi
Jedwali 1: Vyuo vya Ufundi vilivyofutiwa usajili
S/NCHUO
1Institute of Management and Development Studies – Iringa
2Green Hill Institute – Mbeya
3Institute of Business and Social Studies – Mbeya
4Loyal College of Africa – Mbeya
5Mbeya Training College – Mbeya
6Mbengwenya College of Business and Information Technology –Mbinga
7New Focus College – Mbeya
8Shukrani International College of Business and Administration –  Mbeya
9Majority Teachers College – Mbeya
10Rukwa College of Health Sciences – Sumbawanga
11MAM Institute of Education – Mbeya
12Belvedere Business and Technology College – Mwanza
13Geita Medical Laboratory Sciences and Nursing Training College – Geita
14Global Community College – Geita
15Muleba Academy Institute – Muleba
16St. Bernard Health Training Institute – Katoro, Geita
17Victoria Institute of Tourism and Hotel Management – Mwanza
18Gisan Institute of Health Sciences – Mwanza
19Dar es Salaam Institute of Business Management – Dar es Salaam
20SAMFELIS College of Business Studies – Dar es Salaam
21Ellys Institute of Technology – Bunda, Mara
22Tanzania Institute of Chartered Secretaries and Administrators – Arusha
23Emmanuel Community College – Kibaha
24Modern Commercial Institute – Dar es Salaam
25Marian College of Law – Dar es Salaam
Jedwali 2: Vyuo vya Ufundi vinavyotoa mafunzo ambayo hayajathibitishwa
S/NCHUOMAFUNZO
1MISO Teachers College – MafingaCompetence Building Network (CBN) – a Certificate in Early Childhood Education
2Tusaale Teachers College – MafingaCompetence Building Network (CBN) – a Certificate in Early Childhood Education
3The St. Joseph’s College Institute of Business and Management (SJCIBM) – Morogoro
4The Golden Training Institute – Dar es Salaam
5Nkrumah Mkoka Teachers College – Kongwa, Dodoma
6National Institute of Agriculture (Chuo cha Kilimo cha Taifa) – Arusha
7Musoma Utalii Training College – Musoma
8Mwanza Polytechnic Institute – Mwanza
9Mwanza Polytechnic Institute – Maswa
10Ruter Institute of Financial Management – Mwanza
11Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Mwanza
12Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Geita
13Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Bukoba
14Singni International Training Institute – Bukoba
15Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Kahama
16Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Simiyu
17Richrise Teachers College – Geita
18Twiga Training Institute – Musoma
19Zoom Polytechnic Institute – Bukoba
20St. Thomas Training College – Shinyanga
Jedwali 3: Vyuo vya Ufundi vyenye Vituo vya Satellite / Kampasi
S/NCHUO
1MISO Teachers College – Mafinga
2Rungemba Teachers College – Mafinga
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO