Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MEYA WA JIJI LA ARUSHA KALISTI LAZARO AWATUNUKU VYETI WANAHABARI NA KUISHAURI SERIKALI KUANGALIA UPYA SHERIA YA HABARI


 Na Ferdinand Shayo,Arusha .

Meya wa Jiji la Arusha Kalisti Lazaro amewatunuku zaidi ya wahitimu 50 waliohitimu katika Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji  (AJTC) huku akiwataka kuwa mstari wa mbele katika kupigania haki za jamii na kuleta mabadiliko kupitia kalamu zao.

Kalisti amewataka Wanahabari kujikita katika kuandika habari za kijamii zitakazosaidia kutatua changamoto zinazoikabili jamii na kuleta suluhu kwenye matatizo ya jamii.

Ameishauri serikali kuangalia upya mswada wa habari na kuufanyia marekebisho katika vipengelea ambavyo vinaminya haki ya habari.

Mkurugenzi wa Mafunzo katika Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji ,Joseph Mayagila amesema kuwa tasnia ya habari ni tasnia muhimu katika kuchochea maendeleo ya nchi kwani bila taarifa hakuna maendeleo.

Alisema kuwa ni vyema serikali ikatazama upya utekelezaji wa sheria mpya na kufanyia kazi mapungufu ili wanahabari waendelee kuwahabarisha Watanzania

Meya wa jiji la Arusha Kalisti Lazaro akizungumza katika Mahafali ya Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji  Arusha (AJTC) ,Kulia ni Mkurugenzi wa Mafunzo katika Chuo hicho Joseph Mayagila,kushoto ni Diwani wa kata ya Themi ,Melans Kinabo. Picha na Ferdinand Shayo


Wahitimu wa Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji  Arusha (AJTC) wakirusha kofia juu ishara ya kuonyesha kutunukiwa vyeti vya Shahada na Stashahada

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO