Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Taswira: Makamu wa Rais,Samia Suluhu Hassani alitembelea kiwanda cha Mafuta ya Alizeti Mt. Meru Millers Limited cha jijini Arusha jana

Makamu wa Rais,Samia Suluhu Hassan akisikiliza maelezo ya malighafi inayotumika katika kutengenezea mafuta yatokanayo na alizeti katika kiwanda cha Mt. Meru Millers, jijini Arusha.

Makamu wa Rais,Samia Suluhu Hassani ametembelea kiwanda cha Mt. Meru Millers Limited  cha jijini Arusha kinachojishughulisha na utengenezaji wa mafuta yatokanayo na alizeti.

Akizungumza baada yakujionea uzalishaji wakiwanda hicho,amesema lengo kubwa ya ziara yake katika kiwanda hicho ilikuwa nikujionea shughuli zinazofanywa na kiwanda hicho.

Pia ameweza kusikiliza changamoto mbalimbali zinazozikabili kiwanda hicho na kubwa ikiwa ni utozwaji wa kadi nyingi na serikali itahakikisha kunakuwa na utaratibu mzuri wa ulipaji wa kodi hizo.

Aidha alisisitiza zaidi kuwa serikali ya awamu wa tano imedhamilia ujenzi wa viwanda vingi nchini ambavyo vitatumia malighafi za ndani ya nchi nakukuza uzalisha kwa wakulima na hata pia kutoa ajira za kutosha.

Mkurugenzi Mtendaji wa Mt. Meru Millers Atul Mittal alisema ikiwa serikali itapunguza kodi hizi nyingi itasaidia ukuwaji wa viwanda vilivyopo na hata kuhamasisha wawekezaji wengine kuwekeza kwenye viwanda hapa nchini.

Makamu wa Rais yupo Mkoa Arusha kikazi kwa mda wa siku 3 ambapo atendelea kutembelea viwanda vya mkoani  hapa na pia atazindua jengo la Mahakama ya Afrika.

Makamu wa Rais,Samia Suhulu Hassan akiangalia moja ya kifungashio cha mafuta ya alizeti kilichotengenezwa na kiwanda cha Mt,Meru Millers,Arusha.

Makamu wa Rais,Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa Mkoa na wafanyakazi wa kiwanda cha Mt.Meru Millers,jijini Arusha.

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO