Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Shauri la Rufaa Kuhusu Dhamanaya Mbunge Lema Kusikilizwa Jumatatu Novemba 28, 2016 Mahakama Kuu Arusha

Rufaa ya Dhamana ya Mbunge wa Arusha Mjini Mh Godbless Lema anayeendelea kusota rumande kwa dhamana yake kuzuiwa na Serikali kutokana na mashitaka ya kutoa maneno ya uchochezi kwa Rais Magufuli imepangwa kusikilizwa siku ya tarehe 28/11/2016 mbele ya Jaji Mwandamizi wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, Jaji  Fatma Masengi.

Maombi hayo ya rufaa namba 112/113 yalisajiliwa katika Mahakama hiyo jana Novemba 23, 2016 na Mawakili kutoka TANAFRICA LAW wakiongoozwa na Wakili Peter Kibatala kutokana na makosa ya kisheria yaliyofanywa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha.

Awali mawakilihao na mteja wao walipwa maelekezo na Mahakama Kuu walikolalamika na kuomba marejeo ya hukumu ya Hakimu Mkazi wakidai Hakimu Desdery Kamugisha alikosea kisheria kuruhusu rufaa ya mawakili wa serikali kuweka zuio la dhamana ilhali alisharuhusu dhamana kwa mshitakiwa na kwamba ni masharti ya dhamana tu ndio yaliyokuwa ynasubiriwa.
Picha ya Makataba: Lema na wafuasi wake wakitoka katika viwanja vya Mahakama Kuu Arusha wakati akifuatilia kesi yake ya Ubunge miaka ya nyuma

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO