Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

UZINDUZI WA KISMAT ADVERT MEDIA WAFANA JIJINI ARUSHA





Mkurugenzi wa Kismarty Advert Media Company Ltd, Mary Kismart Mollel akiwa anazungumza siku ya uzinduzi wa kampuni hiyo katika ukumbi wa ukumbi wa Asili Resort uliyopo jijini Arusha.

Mkurugenzi wa Kismarty Advert Media Company Ltd ,akiwa anasalimiana na viongozi mbalimbali waliohudhuria katika hafla hiyo katika ukumbi wa Asili Resort iliyopo jijini Arusha

Wa kwanza kulia ni Meya wa jiji la Arusha Calist Lazaro ,akifuatia na aliyeko kulia kwake ni mkuirgenzi wa Kismarty Advert,akifaria na aliyeko kulia kwake ni Dotto Kimaro siku ya uzinduzi wakampuni hiyo.iliyofantika katika ukumbi wa Asili Resort iliyopo jijini Arusha.

Mchekeshaji Steve Nyerere nae hakubakia nyuma alikuwepo akifanya yake katika uzinduzi wa Kismarty Advert Media,.iliyofantika katika ukumbi wa Asili Resort iliyopo jijini Arusha.
Watatu kutoka kushoto ni Meya wa Jiji la Arusha Calist Lazaro ,akifuatiwa na msaidizi meya Viola Lazaro ,aliyepo kushoto kwake ni diwani wa kata ya Themi Kinabo akifuatiwa na Diwani wa kata ya Ngarenaro Nathaniel Nanyaro katika uzinduzi wa Kismarty Advert  Media,iliyofantika katika ukumbi wa Asili Resort iliyopo jijini Arusha.
Mameneja wa Venus Hotel wakiwa katika picha ya pamoja katika uzinduzi wa wa Kismarty Advert Media Company ltd.
Mkurugenzi wa Kismarty Advert Media Company Ltd, Mary Kismart akikata keki kwa kushirikiana na Meya wa Jiji la Arusha Calist Lazaro wakati wa uzinduzi wa kampuni hiyo ya matangazo.iliyofanyika katika ukumbi wa Asili Resort iliyopo jijini Arusha.

Keki ya ndafu nayo ilikuwepo katika hafla hiyo ya uzinduzi wa Kismarty Advert Media Company Ltd .


Mambo haya nayo hayakosekaniki katika hafla kama hii shampein ikifunguliwa hapa na  mmoja wa waandishi wa habari wa kituo cha TV jijini Arusha Millan Cable Hamza Kalemela ,pamoja na mwandishi wa habari kutoka gazeti la Mwananchi communication Zulfa Musa.iliyofantika katika ukumbi wa Asili Resort iliyopo jijini Arusha.Mambo yakiendelea kama uonavyo hapo pichani
Afisa uhusiano  wa Kismarty Advert Media  Company LTD,Gadiola Emmanuel akipongezana na Mkurugenzi wa Kismart Advert Media company ltd,iliyofantika katika ukumbi wa Asili Resort iliyopo jijini Arusha. Wakiwa wanapongezana katika uzinduzi wa Kismarty Advert Media Company ltd ,iliyofantika katika ukumbi wa Asili Resort iliyopo jijini Arusha.

Na Vero Ignatus Arusha.


Meya wa Jiji la Arusha amesema kuwa ni vyema kusapoti na kuyapa kipaumbele mambo mazuri yanayofanyawa na wazawa haswa kwa uthubutu wao wa kufanya mambo ya maendeleo .

Ameyasema hayo katika uzinduzi wa kampuni ya matangazo inayojulikana kama Kismarty Advert Media company ltd , iliyofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa Asili Resort iliopo katika Jiji la Arusha na kuhudhuriwa na wamiliki wa makampuni mbalimbali hapa nchini.

Meya huyo amewataka wananchi kuwa na tabia ya kutangaza biashara zao kwani bila kufanya hivyo hata kama bidhaa itakuwa na uzuri kiasi gani hakuna atakayefahamu thamani yake bila kuitangaza ndipo ifahamaike.

"Jengeni tabia ya kutangaza biashara zenu na bidhaa mnazokuwa nazo ndugu zangu biasahara ni matangazo msikae kimya,ukizingatia hii ni kampuni ya kitanzania,tuache kukuza vya watu tutukuze vya kwetu ndugu zangu "alisema meya.

"Mnapoona kampuni kama hii ya matangazo ndiyo fursa yenyewe hii ya kuitumia kuzitangaza biashara zenu,ukikaa kimya hakuna mtu anayeweza kuifahamu bidhaa yako au biashara yako hata kama unauza vitu vuzuri kiasi gani" alisema Meya.

Kwa pande wake mkurugenzi wa Kismarty Advert Media Company ltd ,bi Mary Mollel amesema kuwa kampuni hiyo inapokea matangazo ya aina mbalimbali na kwa bei ambayo mteja atakayoimudu .

Hivyo amewataka wafanyabiashara biashara mbalimbali kutokuwa waoga kutangaza biashara zao kwani ndiyo njia pekee itakayowasaidia biashara zao kufahamika zaidi na kupata wateja zaidi.

"Msiwe waoga kuthubu kutangaza biashara zenu hapa tunasaidiana wewe unaleta tangazo nakutangazia kwa bei nzuri na wakati huohuo unapata wateja kwa upande wako ,kwa maana nyingine tunawezeshana karibuni sana. " alisisitiza bi Mary.











Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO