Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

VANESSA, DUMISHA HERI WAENDELEA KUSOTA POLISI KWA TUHUMA ZA DAWA ZA KULEVYA

Kamanda Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi (CP), Simon Sirro akizungumza na waandishi wa habari juu operesheni mbalimbali zilizofanyika na jeshi hilo kwa wiki moja leo jijini Dar es Salaam.
Kamanda Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi (CP), Simon Sirro akionyesha dawa za kulevya zilizokamatwa katika operesheni leo jijini Dar es Salaam.
Kamanda Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi (CP), Simon Sirro akinyesha gari lililokuwa linatumika kwa ajili ya utapeli na magari yaliyokamatwa kwa tuhuma mbalimbali leo jijini Dar es Salaam.
Kamanda Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi (CP), Simon Sirro akionyesha pikipiki zinazopita katika barabara ya mabasi yaendayo haraka leo jijini Dar es Salaam.
Kamanda Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi (CP), Simon Sirro akionyesha bunduki iliyoteleekezwa na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi leo jijini Dar es Salaan.picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.


Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limesema linawashikilia watuhumiwa wawili wanaojihusisha usambazaji wa dawa kulevya pamoja na utumiaji wa dawa hizo.
Wanaotuhumiwa na usambazaji wa dawa za kulevya na utumiaji ni mwanamziki Vanessa Mdee na Dumisha Heri ambao wamekamtwa na polisi hivi karibuni.
Akizungumza leo na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kamanda Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi (CP), Simon Sirro amesema wasanii hao walikamatwa hivi karibuni katika mazingira ambayo hakutaja kutokana na masuala ya kiupelelezi.
Amesema kuwa 
baada ya kukamilika kwa upelelezi watafikishwa mahakamani kujibu mashataka yanayowakabili.
Wakati huo huo Jeshi la Polisi linawashikilia watu wanaojihusisha na utapeli kwa kutumia vicoba kuhusisha majina ya Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP , Dk. Reginald Mengi ,Mke wa Rais Mstaa na Mbunge, Salma Kikwete pamoja na Mbunge wa Kawe, Halima Mdee.
Amesema kuwa matapeli hao wametengeneza mtandao wa Focus Vicoba ambao watu wakiingia katika mtandao huo wanakuta taarifa mbalimbali zikiwemo za viongozi na watu wenye uwezo wa kifedha kuwa ndio wanaoendesha Vicoba hiyo kwa kutumia namba za simu za 0757 308381 na 0768 199359 ambazo sio namba za viongozi hao.
Kamishina Sirro amesema kuwa mwaka jana walimkamata Boniface Samson Ojwando (27) kwa tuhuma za kuhusika katika matandao huo na kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu kwa mtandao wa kijamii.
Kamanda Sirro amesema matapeli wengine walikuwa wanatumia gari zenye namba usajili T 400 CNC aina ya Toyota Mark II Grand katika maeneo ya Sinza kwa madai kuwa linauzwa baada ya na baada kukubaliana maziano hufanya uhalifu wa kupora fadha hiyo iliotaka kununulia gari hilo.
Katika hatua nyingine jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es Salaam limekusanya zaidi ya milioni 840 za makosa mbalimbali ya usalama Barabarani
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO