Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

TASWIRA: RAIS BARACK OBAMA ALIVYOWASILI JIJINI DAR ES SALAAM

Rais Barraka Obama akishuka na mtoto wake mkubwa Mallya, uwanjani hapo, jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuanza ziara yake ya siku mbili nchini.

Mke wa Rais wa Marekani, Barrack Obama, Michelle Obama, akishuka kwenye ndege hiyo na mtoto wake, Sasha.

Ndege ya Rais wa Marekani, Barrack Obama, 'Airforce One' ikiwa imetua tayari, uwajani hapo.

Mke wa Rais wa Marekani, Barrack Obama 'First lady' akikumbatiana na Rais Jakaya Kikwete, mara baada ya kuwasili uwanjani hapo na mumewe (kulia), leo mchana.

Rais Obama akipokea maua kutoka kwa mtoto Zakia Minja, uwanjani hapo.

Rais Barrack Obama akiongozana na mwenyeji wake, Rais Jakaya Kikwete mara baada ya kuwasili uwanjani hapo jana mchana.

Rais Obama akikagua gwaride lililoandaliwa kwa ajili yake mara baada ya kuwasili na kupigiwa mizinga 21.

Rais Obama akitoka kukagua gwaride lililoandaliwa kwa ajili yake mara baada ya kuwasili na kupigiwa mizinga 21, uwanjani hapo jana.

Rais Barrack Obama akiwa na mwenyeji wake, Rais Jakaya Kikwete akipokea gwaride la heshima uwanjani hapo, mara baada ya kuwasili jana mchana.

Rais Barrack Obama akisalimiana na mke wa Rais Kikwete, Mama Salama mara baada ya kupokea gwaride la heshima uwanjani hapo.

Rais Barrack Obama, akisalimiana na Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein.

Akisalimiana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd.

Hapa akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe.

Akisalimiana na Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Didas Masaburi.

Hapa Rais Obama na mwenyeji wake, Rais Kikwete, wakifurahia ngoma ya Mganda ya asili ya Wangoni, mkoani Songea.

Hapa Rais Barrack Obama akiongozana na mwenyeji wake, Rais Jakaya Kikwete kwa ajili ya kuondoka Uwanja wa ndege.

Wananchi wakiwa wamekusanyika nje ya jengo la Ikulu kwa ajili ya kumkaribisha Rais Barrack Obama.

Wananchi waliokusanyika nje ya jengo la Ikulu jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kumkaribisha Rais Barrack Obama,wakipunga bendera za Tanzania na Marekani. 

Maofisa na baadhi ya Wakurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, wakiwa nje ya Ikulu, kumkaribisha Rais, Barrack Obama.

Mke wa Rais Jakaya Kikwete, Mama Salma (kulia), akiwa na mgeni wake, First lady, Michelle Obama, kwenye Ofisi za Wama.

Hapa wakiwa Makumbusho ya Taifa, wakipokea mau kwa ajili ya kuweka kwenye mabaki ya vifaa vilivyolipuliwa na bomu kwenye Ubalozi wa Marekani jijini Dar es Salaam.

Wake hao wa Marais wa Marekani na Tanzania, wakiweka mashada hayo kwenye mabaki hayo kwa ajili ya kuwakumbuka waliopoteza maisha yao kwenye tukio hilo.

Wakiwaombea wahanga hao, mara baada ya kuweka mashada hayo ya maua

picha na mitandao

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO