Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam imekataa rufaa ya kupinga kufutwa kwa shitaka la Kutakatisha Fedha linalowakabili Harry Kitilya, Shose Sinare, Sioi Solomoni

MwanaHalisiOnline wanaripoti...
Kutoka kushoto, Sioi Solomoni Sumari, Harry Kitillya na Shose Sinare
Akitoa uamuzi huo Moses Mzuna, Hakimu Mfawidhi Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam amesema kuwa, rufaa hiyo haina mashiko kisheria.
“Rufaa ya shitaka hili haina miguu” amesema Hakimu Mzuna wakati akitoa uamuzi wa rufaa hiyo.
Hakimu Mzuna amesema kuwa, hoja ya upande wa utetezi ya kueleza kuwa, Mahakama Kuu haina mamlaka ya kusikiliza rufaa hiyo kutokana kesi hiyo bado haijafika mwisho na kwamba, Mahakama ya Kisutu iliweza kusikiliza kesi hiyo.
Hakimu Mzuna amefuta rufaa hiyo na kwamba, kesi hiyo itaendelea katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Hakimu Mzuna amemshauri Timon Vitalis, Wakili Mkuu wa Serikali kuendelea na kesi hiyo na kwamba, endapo kesi itafika mwisho wakiwa hawajridhika na uamuzi, wanaruhusiwa kukataa rufaa.
Hata hivyo Mzuna amesema kuwa, upende wa mashitaka wanayo mamlaka ya kubadili hati ya mashtaka
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO