Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Sombetini kwa Bananga wafunga barabara wakidai matuta kuzuia mwendo kasi, Jiji laingilia kati na kuahidi matuta ndani ya siku 5

Mgogorouliosababishwa kufungwa kwa barabara ya Sokomjinga - Ngusero na wananchi wenye hasira umepata ufumbuzi baada ya madiwani wa Kata  Mbili zinazotumia barabara hiyo, Mh Ally Bananga wa Kata ya Sombetini  na Elirehema Nko wa Osunyai wakiwa na Mstahiki Meya wa Jiji Kalisti Lazaro na maafisa wa ujenzi Jiji kufika eneo la tukio kusikiliza wananchi hao na kuahidi kuweka bumps na alama za barabarani kupunguza janga la ajali lililokatisha maisha ya watu wa eneo hilo kwa kugongwa na magari.

Katika msafara huo wa viongozi, Katibu Tawala Wilaya ya Arusha Mjini alimwakilisha DC Nkurlu. Wengine ni maafisa wa polisi na wenyeviti wa serikali za mitaa ya Simanjiro na Banda Mbili walishiriki.

Kwa mujibu wa maelezo ya Mstahiki Meya wa Jiji, matengenezo hayo yatachukua siku tano kukamilika.

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO