Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

SUMAYE ATEULIWA KUWA MJUMBE WA KAMATI KUU CHADEMA


CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimemteua Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu.

Uamuzi huo unatokana na kikao cha Kamati Kuu kilichoketi mjini hapa kwa siku mbili.

Akizungumza na waandishi wa habari Naibu Katibu Mkuu Zazinzar, Salum Mwalimu alisema kwa mujibu wa katiba ya chama hicho, Mwenyekiti wa chama, Freeman Mbowe ana mamlaka ya kuteua majina sita ya wajumbe wateule.

Alisema katika kikao hicho mambo mengi yamezungumzwa lakini pia kuna mambo ya kimkakati hasa katika kuelekea kumaliza mwaka huu na kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na hata uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Mwalimu alisema katiba yao ya mwaka 2006, inazungumzia wajumbe wateule wasiozidi sita ambao watapendekezwa na mwenyekiti wa taifa kwa kushauriana na katibu mkuu na kuridhiwa na vikao.

Alisema Mwenyekiti wa taifa wa chama hicho ametumia kipengele hicho kupendekeza jina la Sumaye kuwa mjumbe wa kamati kuu na jina hilo liliungwa mkono na kikao na kuafikiwa na kamati kuu.

CHANZO: CHADEMA BLOG
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO