Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Marumizi Mabaya ya Mitandao na Ubakaji: 11 Kupandishwa Kizimbani

Jumla ya watu 11 wanaoshikiliwa na Jeshi la  Polisi Mkoani Morogoro kwa tuhuma za kumbaka msishana mwenye miaka 21, kumrekodi na kusambaza picha hizo za video mtandaoni wanatarajiwa kufikishwa Mahakaman hii leo  kujibu mashtaka yanayowakabili.

Kwa mujibu wa Nipashe, Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, Ulirch Matei alieleza jana  kuwa watuhumiwa hao wanafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.

Kamanda huyo  amewataka wananchi kutambua kuwa sheria ya matumizi yw mitandao ipo  na inafanyakazi na hivyo kuacha kusambaza picha chafu wanazopokea kupitia simu za mkononi.

Kamanda Matei alisema watuhumiwa wawili walimbaka na na kumrekodi picha za video msichana huyo  bila ridhaa yake Aprili 28 mwaka huu 1 usiku katika nyumba ya kulala wageni ya Titii iliyopo eneo la  Dakawa wilayani Mvomero  na kisha wakazisambaza picha hizo kwenye mitandao ya kijamii ambapo watuhumiwa wengine 9 wao walishiriki kuzipokea na kuzisambaza pia.

Akifafanua zaidi alisema msichana huyo  alipigiwa simu na mmoja wa watuhumiwa hao Zuber Thabit, anayedaiwa kuwa na uhusiano nae akimtaka aende katika nyumba hiyo ya kulala wageni na kwamba mdada huyo  alipoingia chumbani alimkuta thabiti ameshika kisu na kumuamuru kufanya kila atakachoambiwa huku akimsisitiza kutopiga kelele wala kutoa siri vinginevyo angeuawa.

Mtuhumiwa mwingine aliyeshiriki ukatili huo ni Iddy Adam (30) ambaye ndiye aliyefanyakazi ya kurekodi video hiyo.

Watuhumiwa wengine ni  pamoja Rajab Salehe (26) mkazi wa Dakawa ambaye alikuwa mtu  wa kwanza kutumiwa picha hizo na kuzisambaza kwenye mitandao ya kijamii.

Wengine waliokamatwa kwa kusambaza video hiyo ya udhalilidhaji ni Said Athumani (26), Musini Ngai (36), Said Mohammed (24), John Peter (24), Hassan Ramadhan (27), Ramadhani Ally (26), Lulu Peter (38) na Magreth Njonjome (30) wote  wakazi wa tarafa ya Dakawa. 


Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO