Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MH JOSHUA NASSARI ATEMBELEA SHULE YA SEKONDARI KIKATITI ARUMERU MASHARIKI NA KUJIONEA UHARIBIFU WA MOTO MABWENINI, ATOA MSAADA NA KUFARIJI WAHANGA


Mbunge wa Arumeru Mashariki Mh Joshua Nassari amelazimika kukosa ushiriki wa vikao vya Bunge vinavyoendelea mjini Dodoma na badala yake kulazimika kurudi Jimboni kwake ili kusaidia kufariji wanafunzi, walimu na wazazi kufuatia kuungua moto kwa bweni la wavulana katika Shule ya Sekondari Kikatiti.

Katika ajali hiyo ya moto hakuna mwanafunzi aliyeuumia au kupoteza maisha. Blogu hii haijaweza kupata thamani halisi ya hasara ya moto huo. Tunaendelea kufuatilia na tutakujuza hapahapa.

Katiba bandiko lake kwenye mtandao wa Facebook Mh Nassari ameandika haya

"Natoa pole nyingi kwa Shule ya Kikatiti Sec. kwa janga la kuungua bweni la wavulana.
Nimelazimika kuacha bunge kuja kuwaona. Tunamshukuru sana Mungu kwakuwa hakuna mwanafunzi aliyejuruhiwa wala kupoteza maisha. Together we stand, together we go"
Mh Joshua Nassari akifurahia jambo na baadhi ya wanafunzi wa Sekondari ya Kikatiti 

Mh Nassari akizungumza na walimu na wanafunzi wa Sekondari ya Kikatiti alipoenda kutoa msaada na kufariji wahanga

Sehemu ya bweni la wavulana liliotekekezwa kwa moto. Pichani baadhi ya mafundi wakiendelea na ukarabati wa paa ambalo lilimalizika kabisa

Mh Nassari akiangalia uharibifu wa moto kwenye bweni la wavulana Sekeondari ya Kikatiti

Mh Nassari akifurahi pamoja na wanafunzi wa Sekondari ya Kikatiti baada ya kuwakabidhi misaada ya kibinadamu yakiwemo magodoro na shuka kufuatia bweni la wavulana kuungua na moto

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO