Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Nape Nnauye: Watanzania hawawezi kutuelewa, na Tusipokuwa Makini Hawataturudisha 2020

Mbunge wa Mtama, Mh Nape Nnauye amefunguka na kusema hatua mbalimbali zilizochukulia na serikali ikiwepo kubana matumizi, kufukuza wafanyakazi hewa, kuongezeka kwa mapato kama hazita tafsiriliwa kwa maboresho ya huduma za jamii ni sawa na kazi bure.

Nape Nnauye alisema hayo juzi wakati akichangia katika bajeti ya Wizara ya Maji na kusema serikali inapaswa kufanya mambo kwa kuwafurahisha wananchi kwa kuwapa huduma bora na si vinginevyo.

"Serikali ya awamu ya tano ilipoingia madarakani ilianzakuchukua hatua kadhaa za kuongeza mapato ya serikali, ikiwa ni pamoja na kubana mianya ya wakwepa kodi lakini kupunguza matumizi ikiwemo kupunguza safari, kupunguza sherehe na matumizi ambayo kiukweli kwa namna nyingine yalionekana si ya lazima, ikiwemo kushughulika na wafanyakazi hewa. 

"Lakini pia kwa takwimu tunaambiwa uchumi unakuwa kwa asilimia 7.2 haya yote hayatakuwa na maana kama hayata tafsiriliwa kwenye maboresho ya huduma za jamii na hasa maji. 

"Hatua hizi lengo lake lilikuwa kuongeza uwezo wa serikali sasa kama hatua hizi zimechukuliwa na matokeo yake ni chanya tunapaswa tuyaone kwenye ongezeko la huduma za jamii, tusipofanya hivi hatua tulizochukua zitakuwa hazina maana hata kidogo, bajeti iliyopita tulitenga bilioni mia tisa bajeti hii tukiwa tumesimamimia hatua tulizochukua ambazo kiukweli zingeongeza uwezo wa Serikali tunatoka mia tisa na kwenda mia sita, kwa vyovyote vile Watanzania hawawezi kutuelewa" alisema Nape Nnauye

Nape Nnauye aliendelea kusisitiza kuwa wananchi hawawezi kuielewa serikali kama hatua inazochukua haziendi kubadilisha maisha yao ya kila siku, lakini Mbunge huyo alisema tatizo la maji lipo katika kila jimbo nchi hii sema kinachotokea wanapishana ukubwa wa tatizo.

"Ilani hii ya Chama Cha Mapinduzi ndiyo mkataba wetu kati ya CCM na wananchi tusipoitekeleza wananchi hawatoturudisha na huu ndiyo ukweli kwa sababu tuliwaahidi Mh Naibu Spika na bahati mbaya tatizo la maji pamoja na kuwaathiri watu wote lakini wakina mama ambao ndiyo wapiga kura wakubwa wa CCM ndiyo waathirika wakubwa wa tatizo hili ndiyo maana sina mashaka kwamba serikali itasikiliza na kwenda kuongeza pesa" alisema Nape Nnauye 
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO